MFANO WA MWENYE KUMDHUKURU ALLAH NA ASIYEMDHUKURU ALLAH NI SAWA NA MFANO WA MTU ALIYEHAI YA ALIYEKUFA

ANUANI ZA DUA

  Dua baada ya Sala

  Dua za Asubuhi

  Dua za Jioni

  Dua baada ya Udhu

  Dua za kuingia msikitini

  Dua za kuingia nyumabani

     Dua za kuamka

DUA ZA QURAAN

Sala ya Istikhara

Mlango wa Duaa

 FADHILA ZA DUAA

Alhamdulilah Rabil Aalamin. Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu na kumtakia rehma Bwana Mtume Muhammad S.A.W na kuwatakia radhi wasahaba zake wote.

Amma Baad: Ndugu zangu Waislamu inampasa kila muislam azingatie jambo moja kubwa, nalo ni hizi neema nyingi zisizokuwa na mfano alizotuoa Mwenyezi Mungu. Binaadamu tokea anaamka asubuhi mpaka anakuja  kuweka ubavu kulala, basi yumo anakula neema za Mola wake. Wala hawezi kiumbe yeyote yule kukosa neema moja katika neema hizo. Na hakuna anayeweza kuzikanusha wala kuzikataa.

Baada yote hayo, tukawekewa duaa za kumfanya Binaadamu wakati wake wote umo katika ibada, wala usipe wakati akaghafilika, yaane awe kila wakati anazikumbuka neema hizo na kuhu akimshukuru Mola wake. Ndio Mtume wetu S.A.W akatufundisha duaa nyingi sana zinazomfanya Muislamu asimsahau Mola wake katika kila wakati anaoutumia. Ndio maana unapoamka tu! jambo la kwanza ni kumshukuru Allah kwa kukuhaisha na kukuamsha tena baada ya kuwa umekufa kifo kidogo. Pamoja na madua mengi mtakayoyaona humu. Uislam.net inajitahidi daima kumuwekea Msomaji kila lilokuwa na faida katika maisha yake. Tafadhalini pitieni milango ya madua na ajaribu kila muislamu kuyasoma kama yalivyopangwa, basi hata atahisi moyo wake unapata utulivu, na Allah humuepusha na matatizo mengi kwa uwezo wake Subhana Wataala.

 

 

(Ee Mola wangu Mlezi! Nizindue niishukuru neema yako uliyo nineemesha mimi na wazazi wangu, na nipate kutenda mema uyapendayo, na uniingize kwa rehema yako katika waja wako wema)

 

Copyright © 2004-2005  www.uislam.net