|
Ndugu zangu Waislamu.. Katika neema kubwa za Mwenyezi Mungu ni
kuwafanyia waja wake wema siku moja takita wiki ili wapate kukusanyika na
kuzungumza yale ambayo huwenda yakawafaa katika maendeleo ya maisha yao.
Ndio ikafaridhishwa Sala ya Ijumaa, ambayo huja faridha badala ya
Adhuhuri.
Vipi Husaliwa: Sala ya Ijumaa ni Rakaa mbili. Kwanza huanza
Imamu kutoka Khutba, kisha baada ya khutba ndio muadhini anaqimu
Salaa ya Ijumaa. Imamu husalisha na kusoma kwa sauti katika zote
rakaa mbili, ni sunna kusoma katika Rakaa ya kwanza Suraul (Sabihisma
rabika.. na rakaa ya pili Hal Ataka Hadithul Ghashiyah). Na katika
hukumu zake haifai kuzungumza wakati Imamu anatoa Khutba, wala
kumwambia mwenzako (nyamaza).
Kasema Mwenyezi Mungu katika Suratil Jumaa Aya ya (9 - 11):
(Enyi mlioamini! Ikiadhiniwa Sala siku ya Ijumaa,
nendeni upesi kwenye dhikri ya Mwenyezi Mungu, na wacheni biashara. Hayo
ni bora kwenu, lau kama mnajua.)
*
(Na itakapo kwisha Sala, tawanyikeni katika nchi mtafute fadhila za Mwenyezi
Mungu, na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi ili mpate kufanikiwa.)
*
(Na wanapo iona biashara au pumbao wanayakimbilia hayo na wakakuacha
umesimama. Sema: Yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni bora kuliko pumbao na
biashara. Na Mwenyezi Mungu ni Mbora wa watoa riziki).
Baadhi ya Adabu za
Ijumaa:
Ni vizuri kwa kila
Muislam siku ya Ijumaa kukoga, kama anavyogoka janaba, bali maulamaa
wengine wakasema kuwa ni wajib kwa kila mtu. Kisha vile vile
kuelekea mapema msikitini katika saa ya mwazo ya siku hii ya Ijumaa,
kwani kila ukitangulia ndio fadhila huwa zaidi kama alivyosema Bwana
Mtume (S.A.W). Kisha kuvaa nguo safi na iliyo nzuri ni katika suna
za Siku ya Ijumaa.
Kusikiliza Khutba:
Khutba ya Ijumaa ni
huhisabiwa miongoni mwa hiyo Sala yenyewe, yaani Sala ya Ijumaa
huanzia kwa Khutba, ndio maana ikakatazwa kuzungumza katika ya
Khutba, na atakaezungumza na Imam anatowa khutba basi hana Ijumaa.
Haifai hata kumwambia mwenzako (nyamaza). Wajibu ni kusikiliza
mawaidha kwa makini na kuyazingatia yanayosemwa. Na kuhtba inatakiwa
iwe na anuani muhimu katika yake yanayowakhusu Waislamu pamoja na
kuwafahamisha maendeleo na maisha yao. Na khutba huwa ni mbili hukaa
Imam muda mfupi baina yao.
Ijumaa kwa Wanawake:
Wanawake wa Kiislamu
wanaweza kuhudhuria Sala ya Ijumaa katika Jamaa Msikitini, sharti
wawe mbali na wanaume kusiwe kuna mchanganyiko. Bila ya kurefusha
sauti zao na wakae nyuma ya safu za wanaume au pembeni pamoja na
kuwepo pazia au sitara. |