ADABU ZA KUZUNGUMZA

 

Muislamu anapotaka kuzungumza kwanza kulipima neno lake, lisije likawakera wenzake. Kwani ni haramu Muislamu kumkera Muislamu mwenzake hata kwa maneno. Basi anapokuwa nalo la kusema husema na anapokuwa hana hunyamaza kimya na ndio bora kwake. Na binaadamu neema kubwa kapewa na Mola wake kuweza kuzungumza na kufahamiana na wenzake. Ndio akasema Mwenyezi Mungu katika Surati Rrahmaan Aya ya (1 mpaka 4):

( ÇáÑøóÍúãóÇäõ*Úóáøóãó ÇáúÞõÑúÂäó*ÎóáóÞó ÇáúÅöäÓóÇäó*Úóáøóãóåõ ÇáúÈóíóÇäó)

Maana yake:

          “Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema* Amefundisha Qur’aani* Amemuumba binadamu* Akamfundisha kunena”.

 

Na Uislamu ukabainisha wazi wazi vipi kuitumia neema hii katika kumdhukuru Mwenyezi Mungu kila wakati bila ya kupoteza muda katika mchezo na maneno yasiyokuwa na maana.  Na Uislamu ukapendezea zaidi kunyamaza. Kwani ndio kusalimika na makosa mengi. Ndio Mtume (S.A.W) alisema katika Hadithi iliyotolewa na Imam Ahmad kwa njia ya Abi Dhar Al ghafariy:

( Úáíßó ÈöØõæáö ÇáÕøóãúÊ ¡ ÝÅäøóåõ ãóØúÑóÏÉ ááÔøíúØóÇä ¡ æóÚóæúä áóß óÚóáì ÃóãúÑö Ïöíúäößó )

Maana yake:

          “Jilazimishe sana kukaa  kimya. Kwani huko ni kumfukuza shetani, na hukusaidia katika kutekeleza mambo ya Dini yako.”

Sadakta ya Sayidi ya Rasula Llaah. Kwani binaadamu kila akijishughulisha na maneno mengi akawa kila kitu hutaka kujuwa ndio huwa hana hata wakati wa ibada. Na tabia hii imekatazwa katika Uislamu. Kasema Mtume (S.A.W) katika Hadithi iliyotolewa na Imam Tirmidhiy:

( ãöäú ÍõÓúäö ÅöÓúáóÇãö ÇáúãóÑúÁö ÊóÑúßõåõ ãóÇ áóÇ íóÚúäöíåö )

Maana yake:

          “Katika dalili bora ya Uislamu wa mtu. Ni kuacha yaliyokuwa hayamukhusu.”

 

Jambo madhali halikuhusu basi usilifuatie ukaja ukafedheheka. Mambo ya watu yaache kwa wenyewe. Ila ikiwa katika njia ya kupanisha watu. Lakini sio kila kinachotokea katika nyumba ya jirani yako nawe ukijuwe. Ndio huo umbea! Kutaka kuishibisha roho yako kwa vitu vya watu! Namna hiyo moyo wa Muislamu kabisa utakuwa bado hauko sawa, tena unahitajia matibabu ya hali ya juu kabisa. Ndio Mtume (S.A.W) kasema katika Hadithi  iliyotolewa na Imam Ahmad:

 

( áóÇ íóÓúÊóÞöíãõ ÅöíãóÇäõ ÚóÈúÏò ÍóÊøóì íóÓúÊóÞöíãó ÞóáúÈõåõ ¡ æóáóÇ íóÓúÊóÞöíãõ ÞóáúÈõåõ ÍóÊøóì íóÓúÊóÞöíãó áöÓóÇäõåõ ¡ æóáóÇ íóÏúÎõáõ ÑóÌõáñ ÇáúÌóäøóÉó áóÇ íóÃúãóäõ ÌóÇÑõåõ ÈóæóÇÆöÞóå )õ  

Maana yake:

          “Haitokuwa madhubuti Imani ya mja mpaka unyooke moyo wake. Na haotunyooka moyo wake mpaka unyooke ulimi wake. Na wala hatoingia Peponi yule mtu ambaye hampi uaminifu jirani yake. Kwa yale mabaya anayomtendea.”

 

Wallahi ingelikuwa ulimwenguni yanatazamwa yale wanayoyasema watu, basi yangelikutikana mengi ni maneno ya upuuzi. Wala hayana faida katika maisha yao. Laiti vikao kama hivi vikawa vya kutafuta elimu na kupeana nasaha.  Ndio maana shetani akawa na nguvu za kutosha katika kuwapoteza watu. Kwani vingalikuwa vikao vya Waislamu katika kumtaja Allah, basi shetani maluuni asingelipata wafuasi wengi, ila wale wale tu waliopotoka. Mwenyezi Mungu alaeleza hayo katika Suratil Israa Aya ya (63-64):

 

( æóÇÓúÊóÝúÒöÒú ãóäú ÇÓúÊóØóÚúÊó ãöäúåõãú ÈöÕóæúÊößó æóÃóÌúáöÈú Úóáóíúåöãú ÈöÎóíúáößó æóÑóÌöáößó æóÔóÇÑößúåõãú Ýöí ÇáúÃóãúæóÇáö æóÇáúÃóæáóÇÏö æóÚöÏúåõãú æóãóÇ íóÚöÏõåõãú ÇáÔøóíúØóÇäõ ÅöáøóÇ ÛõÑõæÑðÇ*Åöäøó ÚöÈóÇÏöí áóíúÓó áóßó Úóáóíúåöãú ÓõáúØóÇäñ æóßóÝóì ÈöÑóÈøößó æóßöíáðÇ)

Maana yake:

          “Na wavute uwawezao miongoni mwao kwa sauti yako, na uwakusanyie (jeshi lako la) wapandao farasi na waendao kwa miguu. Na shirikiana nao katika mali yao na watoto wao, na wa’ahidi ahadi za uwongo. Lakini shetani hawapi wa’adi ila wa udanganyifu”.

 

Na Mtume (S.A.W) kasema katika Hadithi iliyotolewa na Imam Al Bukhari:

 

( Åöäøó Çááøóåó ßóÑöåó áóßõãú ËóáóÇËðÇ Þöíáó æóÞóÇáó æóÅöÖóÇÚóÉó ÇáúãóÇáö æóßóËúÑóÉó ÇáÓøõÄóÇáö)

Maana yake:

          “Kwa hakika Mwenyezi Mungu anachukizwa kwenu na mambo matatu. Kuzungumza sana, na kupoteza mali (kwa kufanya israfu) na kuuliza uliza sana mambo ya watu.”

Kwa hivyo Muislamu anapotaka kuzungumza na wenzake, awe mpole sio kuropokwa bila ya faida. Tena kwa adadu nzuri bila kuhamaki na kukunja uso. Ikawa ghadhabu haimwishi katika uso wake.

Copyright ©2004  Uislam.net