Hitimisho

La kushangaza baada ya yote hayo Waislamu tumelinyamazia kimya suala la UKIMWI katika jamii yetu. Tukiangalia miongoni mwa taasisi na mashirika ya Kiislamu hakuna juhudi za kweli na maksudi kukabiliana na UKIMWI ima kwa kuandaa mipango au miradi au kutoa huduma za kimaisha au kiroho kwa waliokumbwa na janga la UKIMWI.

Suala jengine la kujiuliza uko wapi machango wa wanawake wa Kiislamu ? Na vikundi vingapi vya wanawake wa kiislamu vinajishughulisha na taathira za UKIMWI?

Kwa jumla Waislamu bado hatujaanza kulizungumzia suala la UKIMWI na jinsi ya kujinusuru nao. Imekuwa rahisi kujihami na " la takrabu zinaa yaani musikaribie zinaa bila ya KUCHUKUA HATUA ZA VITENDO ZA UJUMBE WA AYA TUKUFU na kuzingatia kwa upande mwengine mazingira na desturi zinopelekea kushamIri kwa mienendo na hulka zinostawisha kuenea kwa UKIMWI Inafaa kwa wakati huu, wa kujitakasa nafsi mtafakari kwa undani zaidi jinsi kunavyokabiliana na janga hili, gonjwa lisilo na dawa wala kinga thabiti.

TAMATI

Copyright ©2004-2005  www.uislam.net