DINI YA HAKI

 

    Jee! Uislamu ni Dini ya haki?

Ndugu zangu Wasomaji madhumuni ya makala au maelezo haya  sio kupinga dini yoyote, wala kumhujumu aliyekuwa si Muislamu, au kumshambulia Muislamu aliyekuwa hafuati Uislamu kama anavyotakiwa. Lakini madhumuni ya maelezo haya ni kuwasaidia wale ambao  wanataka kujisaidia nafsi zao, ambao wanataka kujua na kuufahamu ukweli wa dini hii na umuhimu wa kuifuata na kutekeleza maamrisho ya Mungu mmoja wa haki kwa ajili ya maslaha, mafanikio na faida ya pamoja ya duniani na akhera.

Kwanza itabidi tukubaliane kuwa katika ulimwengu huu tunaoishi hakuna maneno yaliokuwa hai, ya ukweli, yenye maana, yenye uwongofu yaliokuwa madhubuti kama maneno ya Mwenyeezi Mungu. Hili jambo halina wasi wasi wala shaka hata kidogo. Kwa hivyo maneno yaliotajwa na Mola wetu katika kitabu cha mwisho cha viumbe wote ambacho ni Qur’ani, kilicholetwa miaka elfu kumi na nne nyuma. Kitabu hicho bado kipo hai na yataendelea maneno yake kuwa hai, kudumu na kudhihiri ukweli wake na kufahamika zaidi, kwa sababu Mwenyeezi Mungu kachukuwa ahadi ya kukilinda kitabu hicho. (Qur’ani)

Qur’ani ni maneno ya Mwenyeezi Mungu ambayo wajibu wa kila mwenye akili, fahamu, ujuzi na busara kwa Binaadamu na Majini kukiamini na kukifuata kitabu hicho na kuyazingatia na kuyapekecha maamrisho hayo ikiwa tunataka uwongofu, amani, salama ya nafsi zetu na himaya ya maisha yetu kutoka kwa Mola wetu kwa maslaha ya hapa duniani na Akhera.

 Mungu huyo mmoja (wa kweli na wa haki) ni yule yule aliyemteremshia uwongofu Mtume Nuhu, Mtume Ibrahim, Mtume daudi, Mtume Musa, Mtume Issa, Mtume Muhammad na Watume wengineo wote wa mwanzo waliopita. Kwa yoyote asiyewaamini watume hao waliotajwa na Mola wetu basi hajawa Muislamu wa kweli, kwani anapinga maneno ya Mola wake.

 Aya ifuatayo au maneno haya ni kutoka kwenye kitabu kitukufu cha Mwenyeezi Mungu, ambaye anatubainishia kwa kutufahamisha na kutuilimisha waja wake. Kwa hivyo ndugu msomaji nakuusia yasome zaidi ya mara moja na jaribu kuyafahamu na kuyazingatia ili upate faida zaidi.

ÔóÑóÚó áóßõã ãøöäó ÇáÏøöíäö ãóÇ æóÕøóì Èöåö äõæÍðÇ æóÇáøóÐöí ÃóæúÍóíúäóÇ Åöáóíúßó æóãóÇ æóÕøóíúäóÇ Èöåö ÅöÈúÑóÇåöíãó æóãõæÓóì æóÚöíÓóì Ãóäú ÃóÞöíãõæÇ ÇáÏøöíäó æóáóÇ ÊóÊóÝóÑøóÞõæÇ Ýöíåö

Amekuamrisheni (sharia ya) dini ile ile aliyomuusia Nuhu na tuliokufunulia wewe (Muhammad), na tuliowausia Ibrahim, na Musa na Issa, kwamba shikeni dini wala msifarikiane kwa hayo.

Ash-shuura-13

Watume wote walioteremshwa na huyo Mungu mmoja (jina lake Allah) wameteremshwa kwa ajili ya maelekezo yale yale waliokuja nayo Watume waliopita. Na kusisitizwa kuwa hakuna Mungu wa kuabudiwa isipokuwa Mungu mmoja tu. Na ujumbe ni ule ule wa kuwatetea viumbe na kila mabaya na kuwaongoza waliopotea ili washikamane na uwongofu unaotoka kwa Mola wao kwa madhumuni ya kuwa wawe viumbe bora, waweze kuishi maisha mazuri duniani na kupata ujira wa kuishi maisha mazuri Akhera.

 Kwa kuwa Mungu alioteremsha Watume na vitabu vilivyopita ni yule yule ‘Allah’ kwa hivyo hapa inabidi tukubaliane kuwa ‘Allah’ alikuwa kishapanga kuwa atamleta Mtume mwengine baada ya  Mtume Musa na Issa, na kuamua kuwa huyo ndiye atakaekuwa Mtume wa mwisho, ambaye jina lake litakuwa Muhammad (Ahmad), alikuwa kishaweka wapi amweke na lini amkabidhi jukumu la Utume. Aya zifuatazo zinathibitisha hayo.

 Kutabiriwa Mtume Muhammad (SAW) katika Taurat na Injiil

ÇáøóÐöíäó íóÊøóÈöÚõæäó ÇáÑøóÓõæáó ÇáäøóÈöíøó ÇáÃõãøöíøó ÇáøóÐöí íóÌöÏõæäóåõ ãóßúÊõæÈðÇ ÚöäÏóåõãú Ýöí ÇáÊøóæúÑóÇÉö æóÇáÅöäúÌöíáö íóÃúãõÑõåõã ÈöÇáúãóÚúÑõæÝö æóíóäúåóÇåõãú Úóäö ÇáúãõäßóÑö æóíõÍöáøõ áóåõãõ ÇáØøóíøöÈóÇÊö æóíõÍóÑøöãõ Úóáóíúåöãõ ÇáúÎóÈóÂÆöËó æóíóÖóÚõ Úóäúåõãú ÅöÕúÑóåõãú æóÇáÃóÛúáÇóáó ÇáøóÊöí ßóÇäóÊú Úóáóíúåöãú ÝóÇáøóÐöíäó ÂãóäõæÇú Èöåö æóÚóÒøóÑõæåõ æóäóÕóÑõæåõ æóÇÊøóÈóÚõæÇú ÇáäøõæÑó ÇáøóÐöíó ÃõäÒöáó ãóÚóåõ ÃõæúáóÜÆößó åõãõ ÇáúãõÝúáöÍõæäó

 Ambao kwamba wanamfuata huyo Mjumbe, Mtume, asiyesoma wala kuandika, wanayemkuta kaandikwa kwao katika Taurat na Injiil, anayewaamrisha mema na anayewakataza mabaya (maovu), na anawahalalishia vizuri, na anawaharamishia viovu, na anawaondolea mizigo yao, na minyororo iliyokuwa juu yao. Basi wale waliomuamini yeye, na wakamhishimu, na wakamsaidia, na wakafuata nuru iliyoteremshwa pamoja naye, hao ndiyo wenye  kufanikiwa.

Al A’raaf-157

 Maelezo zaidi

Maneno haya ya Mwenyeezi Mungu yanatuonesha dalili zilizo wazi kuwa Mayahudi na Manasara walikuwa wanajua kuwa atakuja Mtume mwengine na utakuja uwongofu wa kitabu changine kwa sababu washaambiwa na Mola wao. Na sababu ya kuambiwa huko ni kuwa wasimpinge na wamkubali na wafuate uwongofu mpya huo utakapofika (Qur’ani).

 Lakini yalipodhihiri hayo wengine hawakukubali, na moja ya sababu ya kutokubali ni kuwa Mtume huyo hakutokana katika wao. Wakubwa hao na wafuasi wao wakaona wakikubali basi itabidi vyeo vyao na mamlaka ya wafuasi wao vitatoweka. Kwa hivyo wakafanya kila njia kupinga na kukataa kufuata na kutii amri ya Mola wao na Mitume wao.

 Sifa hizi za Mtume huyu (Muhammad) asiyejua kusoma wala kuandika, zimetajwa katika aya nyangine vile vile. Na sababu kubwa ni kuonesha dalili kuwa haya yaliokuja hayatoki kwa Muhammad, yeye hana ilimu, si msomi wala muandishi, huu ni ujumbe unaotoka kwa ‘Allah’ kwa hivyo atakayepinga huwa hampingi Muhammad, bali anampinga mwenyeezi Mungu. Ewe Muumbwa! Una uwezo wewe wa kumpinga Muumbaji?

æóãóÇ íóäØöÞõ Úóäö Çáúåóæóì Åöäú åõæó ÅöáøóÇ æóÍúíñ íõæÍóì Úóáøóãóåõ ÔóÏöíÏõ ÇáúÞõæóì

Na wala hatamki kwa matamanio (yake Muhammad). Hayakuwa haya ila ufunuo uliofunuliwa. Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu (Mwenyeezi Mungu).

      Annajm-3, 4, 5

 Kwa hivyo aliyokuwa akiyaleta na kuyafundisha Mtume Muhammad (SAW) ni maamrisho kutoka kwa Mwenyeezi Mungu, sio maamrisho kutoka kwake Muhammad, yeye hakuwa na ilmu ya darja kubwa kama hii, yeye hakuwa mjuzi wala msomi, kwa hivyo ukweli uko wazi, na wapinzani huwa wanampinga Mola.

 Kwa hakika kuja kwa Mtume mpya (Muhammad)  na kitabu kipya (Qur’ani) ilikuwa ni rehma kubwa kwa Mayahudi (wafuasi wa Taurat), Manasara (wafuasi wa injiil) na wengineo, kwani upotofu wa viongozi wao uliwafanya viumbe hawa kuwa wamejitwika mizigo mikubwa na wamejifunga na minyororo ya shida na dhiki. Kwani walikuwa wamejiharamishia mambo wenyewe, wamejiwekea vikwazo vya kimaisha vya kila aina kwa kufuata mila zao, wafuasi wao na kufuata nyao za mababu zao.

 Ama wale waliomuamini aliyokuja nayo Mtume Muhammad (SAW), na wakamuhishimu, na wakamsaidia, na wakafuata nuru iliyoteremshwa kutoka kwa Mola wao, hao ndiyo waliofanikiwa duniani na Akhera. Kwani wameitikia wito wa Mola wao na wametii amri na kufuata uwongofu mpya uliowajia wa Qur’ani.

 Kutabiriwa Mtume Muhammad (SAW) na Mtume Issa (as)

æóÅöÐú ÞóÇáó ÚöíÓóì ÇÈúäõ ãóÑúíóãó íóÇ Èóäöí ÅöÓúÑóÇÆöíáó Åöäøöí ÑóÓõæáõ Çááøóåö Åöáóíúßõã ãøõÕóÏøöÞðÇ áøöãóÇ Èóíúäó íóÏóíøó ãöäó ÇáÊøóæúÑóÇÉö æóãõÈóÔøöÑðÇ ÈöÑóÓõæáò íóÃúÊöí ãöä ÈóÚúÏöí ÇÓúãõåõ ÃóÍúãóÏõ ÝóáóãøóÇ ÌóÇÁåõã ÈöÇáúÈóíøöäóÇÊö ÞóÇáõæÇ åóÐóÇ ÓöÍúÑñ ãøõÈöíäñ

Na Issa mtoto wa Maryam aliposema: Enyi wana wa Israili! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyeezi Mungu kwenu, ninathibitisha yaliyokuwa kabla yangu katika Taurat, na mwenye kubashiria kuja Mtume atakaye kuja baada yangu, jina lake ni Ahmad. Lakini alipo waletea hoja zilizowazi walisema: Huu ni uchawi ulio dhahiri.

Ass’af-6

 Maelezo zaidi

Hapa kuna mambo mawili yanakwenda sambamba, kwanza Mtume Issa anawaambia Mayahudi ambao walikuwa wakifuata Taurat, kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyeezi Mungu, na anayathibitisha na kuyakubali yaliokuja katika Taurat, yaani aliyokuja nayo Mtume Musa. Kwa hivyo wamkubali na wafuate kitabu kipya cha Injiil alichoteremshiwa yeye Mtume Issa.

 Jambo la pili (Mtume Issa) anawabashiria (kwa amri ya Mwenyeezi Mungu) kuwa vile vile kutakuja Mtume mwengine baada yake jina lake Ahmad, kwa hivyo ina maana kwa wakati ule alikuwa akiwalingania wafuate uwongofu mpya wa Injiil, na waache Taurat, na kuwabashiria kuwa ukifika uwongofu mpya baada ya Injiil, wote wafuate uwongofu huo atakayekuja nao huyo Mtume ambaye jina lake Ahmad (Muhammad).

 Mtume alipozaliwa, baba yake alikuwa kisha kufa, mama yake alimpa jina la Ahmad, na baada ya kufa mama yake akachukuliwa kulelewa na Babu yake ambaye akamwita Muhammad, na inasemekana kuwa Ahmad na Muhammad ni jina moja.

Sasa tukirudi tena kwa Mtume Issa, wakati alipo waletea hoja zilizowazi kabisa, wakaona hawana njia ya kuyakimbia isipokuwa walisema: “Huu ni uchawi ulio dhahiri” ili waendelea na mambo waliokuwa wanakwenda nayo, lakini ukweli wanaujua na wanayafahamu uzuri.

Kwa hivyo nawausia ndugu zangu waliokuwa bado hawajaamua kujisalimisha kwa Mungu wa haki, Mungu wa mitume wote waliopita kuwa wasikubali kupotezwa kwa kumuasi Mola wao na Mitume yao. Kwani wamepewa akili na fahamu nzuri ya kuyazingatia haya. Kwa hivyo ni wajibu kuutumia uwezo huo wa fahamu kwa kutafuta njia ya uwongofu ili isifike wakati wakafa na wao bado hawajaamua kujisalimisha kwa Mola wao. Kwani mtu akifa na bado hajarejea kwa Mola wake, basi malipo yake ni moto mkali sana wa milele wenye maumivu makubwa sana.

 Kubashiriwa kuja Mtume Muhammad (SAW) katika Taurat

Þõáú ÃóÑóÃóíúÊõãú Åöä ßóÇäó ãöäú ÚöäÏö Çááøóåö æóßóÝóÑúÊõã Èöåö æóÔóåöÏó ÔóÇåöÏñ ãøöä Èóäöí ÅöÓúÑóÇÆöíáó Úóáóì ãöËúáöåö ÝóÂãóäó æóÇÓúÊóßúÈóÑúÊõãú Åöäøó Çááøóåó áÇó íóåúÏöí ÇáúÞóæúãó ÇáÙøóÇáöãöíäó

Sema: Mwaonaje yakiwa haya ni kweli yanatoka kwa Mwenyeezi Mungu, nanyi mmeyakataa, na akashuhudia shahidi miongoni mwa wana wa Israili juu ya mfano wa haya, na akaamini na nyinyi mnafanya kiburi? Hakika Mwenyeezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu.

Ah’qaaf-10

 Maelezo zaidi

Aya hiyo ya juu inaeleza kuhusu mmoja miongoni mwa Mayahudi  jina lake *Abdallah bin Salaam, ambaye alisilimu, na alipoulizwa kwa nini amesilimu, akasema kwa kuwa Mtume Muhammad (SAW) ametajwa katika Taurat. Lakini wengine wakatakabar na kukataa kuamini. *(Kutoka katika tafsiri ya Attabriy- sababu za kuteremshwa Qur’an)

 Tumeona maelezo na mafahamisho ya aya hizo tulizozipitia, ambazo ni maneno yaliotoka kwa ‘Allah’ (Mwenyeezi Mungu) sio maneno ya Muhammad wala si maneno ya Waislamu. Maneno hayo yanatupa ukweli kuwa Mungu wa Watume wote ni mmoja. Sasa kwa nini tunamkubali Mungu mmoja na hatumkubali Muhammad. Ikiwa imefika hadi Muhammad kutajwa katika Injiil na Taurat, maana yake tumkubali na kumfuata kwa yale yalioteremshwa na Mola wetu.

 Na ikiwa hatufanyi hivyo, basi inamaanisha kuwa hata hivyo vitabu tuliokuwa navyo hatuvifuati na tunavipinga au hatukubaliani na yalioandikwa, na khatari zaidi kuwa tunampinga Mungu wa Watume wote hao tunaowaamini. Kwa hivyo inamaanisha kuwa hatufuati, Taurat, wala Injiil wala Qur’ani. Sasa tunafuata dini gani na Mungu yupi tunayemuamini?

 Ndugu yangu ikiwa hujaamua au kutia nia kujisalimisha kwa Mungu wa haki ‘Allah’ na kufuata kitabu chake cha mwisho Qur’ani, siwezi kusema kuwa umepotea, lakini nakuomba ujionee huruma nafsi yako, viumbe sote tunakosa, lakini makosa ya kumpinga Mwenyeezi Mungu ni makubwa mno na yana hatari kubwa duniani, na majuto makubwa yatakuwa siku unayokufa na ukaondoka duniani umedhalilika na adhabu kali ya moto wa Akhera inakungojea.

 Inahitaji ndugu zangu tufikiri, tuzingatie nafsi zetu, na tuamue kufuata njia ya uwongofu, na tusifuate upotofu. Tusiwe wakaidi na wabaya wa nafsi zetu, kwani tumepewa akili kwa hivyo inatuwajibikia kuitumia kwa kuchukuwa uamuzi wa kheri na wa kweli. Hapa hakuna kuvungana kila kitu kipo wazi kabisa. Ikiwa ndugu yangu bado hujaridhika na yote yaliokuzunguka, basi kuwa mstahamilivu na jitahidi kusoma yanayofuatia ili upate maelekezo zaidi.

Ãóãú ÊóÞõæáõæäó Åöäøó ÅöÈúÑóÇåöíãó æóÅöÓúãóÇÚöíáó æóÅöÓúÍóÜÞó æóíóÚúÞõæÈó æóÇáÃÓúÈóÇØó ßóÇäõæÇú åõæÏðÇ Ãóæú äóÕóÇÑóì Þõáú ÃóÃóäÊõãú ÃóÚúáóãõ Ãóãö Çááøåõ æóãóäú ÃóÙúáóãõ ãöãøóä ßóÊóãó ÔóåóÇÏóÉð ÚöäÏóåõ ãöäó Çááøåö æóãóÇ Çááøåõ ÈöÛóÇÝöáò ÚóãøóÇ ÊóÚúãóáõæäó

 Au mnasema (nyinyi Mayahudi na Manasara) kuwa Ibrahim na Ismail na Is’hak na Yaakub na wajukuu zao waliokuwa Mayahudi au Wakristo? (kama nyinyi) Sema: Je nyinyi mnajua zaidi au Mwenyeezi Mungu? Na ni nani mwenye kudhulumu zaidi kuliko yule aliyeficha ushahidi alionao utokao kwa Mwenyeezi Mungu? Na Mwenyeezi Mungu sio mwenye kughafilika kwa hayo mnayoyafanya.

Al Baqara-140

Maelezo zaidi

Mayahudi na Manasara (Wakristo) hawakupendekezewa kuona kaja Mtume sio katika jamii yao. Ijapokuwa ametabiriwa katika hivyo vitabu wanaosema kuwa ndivyo wanavyovitegemea, kwa hivyo hawakukubali kufuata maelekezo hayo, na mpaka leo wanaendelea na ushindani wao wa kutomkubali Mtume Muhammad (SAW) na kutoikubali Qur’ani inayotoka kwa Mola wao huyo huyo aliyewateremshia Taurat na Injiil.

 Na baada ya kutokubali ukweli wakawa wanapindukia mipaka na kuipinga na kujadiliana, hata kufika hadi kusema kuwa Mitume fulani na fulani wametokana na  katika sisi, yaani wanamtowa makosa Mwenyeezi Mungu kwa nini basi asilete Mtume kutokana na wao, kenda kuleta Mtume  kutokana na jamii ya Warabu, kwa hivyo wao hawamkubali.

Hapa Mwenyeezi Mungu anawauliza kutokana na maneno yao kuwa “Je nyinyi mnajua zaidi au Mwenyeezi Mungu ndiye mjuzi”? Na wakati huo huo Mwenyeezi Mungu katoa onyo kwa kusema ni nani mwenye kudhulumu zaidi kuliko yule aliyeficha ushahidi alionao utokao kwa Mwenyeezi Mungu? Na Mwenyeezi Mungu sio mwenye kughafilika kwa hayo wanayoyafanya. Yeye anajua kila kitu, na atawalipa wanaompinga na kumuasi, kwani yeye haghafiliki wala hasau yanaotendeka.

ÇáøóÐöíäó ÂÊóíúäóÇåõãõ ÇáúßöÊóÇÈó íóÚúÑöÝõæäóåõ ßóãóÇ íóÚúÑöÝõæäó ÃóÈúäóÇÁåõãú æóÅöäøó ÝóÑöíÞÇð ãøöäúåõãú áóíóßúÊõãõæäó ÇáúÍóÞøó æóåõãú íóÚúáóãõæäó

Wale tuliowapa kitabu wanayajua haya kama wanavyowajua watoto wao, na kuna kikundi katika wao huificha haki na hali wanajua.

Al Baqara-146

Maelezo zaidi

Hapa inaonesha wazi kabisa kuwa yote yaliokuja ya haki wanayajua uzuri Mayahudi na Manasara, wanamjua Mungu wa haki, wanajua Qur’ani ni kitabu cha haki, wanajua Muhammad (SAW) ni Mtume wa haki, na wanajua kibla wanachoelekea Waislamu (Al Kaaba) kumuabudu Mola wako ni cha haki, ni moja katika vilivyotajwa katika vitabu vyao.

Baada ya Mtume Muhammad (SAW) kuteremshiwa ujumbe wa kuelekea Al Kaaba wakati wa kusali, badala ya kuelekea Baitul Muqaddas, Mayahudi na Manasara walikasirika na kupendelea Waislamu waelekee huko wanakoelekea wao. Ijapokuwa wanajua na imetajwa katika vitabu vyao kuwa wataelekea Kibla cha Maka, lakini walijifanya kama hawafahamu, na ndio hapo Mwenyeezi Mungu anawafedhehesha kwa kusema kuwa wanayajua hayo yote kama wanavyowajua watoto wao.

Þõáú íóÇ ÃóíøõåóÇ ÇáäøóÇÓõ Åöäøöí ÑóÓõæáõ Çááøåö Åöáóíúßõãú ÌóãöíÚðÇ ÇáøóÐöí áóåõ ãõáúßõ ÇáÓøóãóÇæóÇÊö æóÇáÃóÑúÖö áÇ ÅöáóÜåó ÅöáÇøó åõæó íõÍúíöÜí æóíõãöíÊõ ÝóÂãöäõæÇú ÈöÇááøåö æóÑóÓõæáöåö ÇáäøóÈöíøö ÇáÃõãøöíøö ÇáøóÐöí íõÄúãöäõ ÈöÇááøåö æóßóáöãóÇÊöåö æóÇÊøóÈöÚõæåõ áóÚóáøóßõãú ÊóåúÊóÏõæäó

Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume kwenu nyinyi nyote, niliyetumwa na Mwenyeezi Mungu, Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Hapana Mungu ila yeye anayehuisha na anayefisha. Basi muaminini Mwenyeezi Mungu na Mtume wake asiyejua kusoma na kuandika, ambaye anamuamini Mwenyeezi Mungu na meneno yake. Na mfuateni yeye ili mpate kuongoka.

Al A’raaf-158

Maelezo zaidi

Hapa kwanza mwenyeezi Mungu anamuamrisha Mtume Muhammad (SAW) kuwa awaambie na kuwafahamisha watu kuwa yeye ni Mtume wa wote, yaani Mtume wa Waarabu, Mayahudi, Manasara na wengineo wote, ni Mtume wa ulimwengu wote. Yaani inamaanisha kuwa hakuna kufuata kitabu cha uwongofu isipokuwa Qur’ani tu, na kumfuata Mtume wa mwisho tu.

Mtume huyo na kitabu hicho kimeteremshwa na Mfalme wa mbingu na ardhi, mwenye kuhuisha viumbe na mwenye kufisha. Basi tunatakiwa tumuamini yeye Mwenyeezi Mungu na Mtume wake asiyejua kusoma wala kuandika, ambaye yeye anamuamini Mwenyeezi Mungu na maneno yake (Qur’an) Vipi leo watu wamesoma wanaandika na wanayafahamu yote hayo na hawataki kufuata haki? Mola wetu anatuamrisha tumfuate yeye Muhammad ili tupate kuongoka, kufaidika na kufanikiwa duniani na Akhera.

Matatizo ya kutoufahamu Uislamu

Baadhi ya watu hasa wale wasiokuwa Waislamu ambao hawaufahamu Uislamu, kwa hivyo wanachukulia kuwa hii ni dini ya vikwazo vinavyowazuilia watu uhuru wa maisha yao, au ni dini ya watu waliokuwa hawajaendelea kimaisha, au ni maadui wanaotaka kuangusha dini nyangine na kuifanya dini ya Kiislamu kuwa ndio bora kuliko dini nyengine zote.

 Ni kweli kabisa dini hii ni bora na ndio inayotakiwa kufuatwa na wote. Na inajuulikana wazi kabisa kuwa dini zilizopita mikono ya viumbe imekwisha badilisha maneno ya Allah kwa kuyapunguza na kwa kuyaengeza, na ndio sababu ya kuja kitabu kipya na Mtume mpya. Ndugu zangu tukipenda au tukichukia ndivyo hivyo hivyo hakuna jengine jipya. Ikiwa watu hawataki kuongoka na kukubali ukweli, basi wajuwe kuwa watu wanasonga mbele kufuata nuru ya uwongofu na wapinzani  wanabakia  kizani kufuata njia zao za upotofu.

 Upotofu unatokana na mambo mawili, kwanza ni kutoufahamu nini Uislamu na wengine kutotaka kuufahamu Uislamu. Jambo la pili ni kuwa wapo vile vile wanaoufahamu Uislamu nje na ndani, lakini wanafanya vitimbi vyao. Kwa hivyo wanafanya mambo ya maslaha ya kidunia ambayo matokeo yake ni kujenga ukuta wa chuki na upotofu, na madhara makubwa ni kuwa viumbe wanajipotowa na wanawapoteza wenzao.

 Na kwa wale waliokuwa si Waislamu ambao hawakupata fursa ya mafahamisho ya kweli na kuufahamu ukweli huu wa dini hii ya huyo huyo Mungu mmoja anayeabudiwa na wote, basi inakuwa ni vigumu kwao kuujua ukweli na wanatishwa na maadui wa Uislamu na kutiwa chuki hata kufikia hadi kuhisi kusalimiana na ndugu zao, jirani zao waliokuwa Waislamu inakuwa kwao ni jambo zito lisilokuwa na budi.

 Kwa hivyo madhumuni ni kujaribu kuelezana mambo kwa mpango maalumu ili wale waliokuwa si Waislamu waweze kuujua na kuufahamu Uislamu kwa hoja na majadiliano ya kiakili kwa kusoma yaliokuwa muhimu kuyajua na kuyazingatia ili waweze kuyapima na kuyakubali kwa imani yao, na kwa uhuru wa nafsi zao. Katika Uislamu hakuna kulazimishwa mtu kujisalimisha nafsi yake kwa Mola wake,  bali ni hiyari ya nafsi ya kujitoa kwenye kiza cha upotofu na kujiingiza kwenye nuru ya uwongofu.

 Kwa hivyo iwapo kutakuwa na mafahamisho ya busara, na maelekezo yenye msingi madhubuti, wengi waliokuwa si Waislamu wanaojihurumia nafsi zao kwa kutaka kufuata haki na kujiepusha na matatizo ya duniani na Akhera, utawakuta wanajisalimisha kwa Mola wao, kwa sababu wamekwishaona nuru ya ukweli na utamu wa uwongofu wa kufuata haki.

 Na wapo wale Waislamu ambao hawaufahamu udani wa Uislamu, ambao vile vile wakipata maelekezo mazuri hubadilika na kuwa wenye kutimiza walioamrishwa na kuwacha waliokatazwa, na kujitoa katika ghadhabu za Mwenyeezi Mungu na kujiweka katika kundi la vipenzi vya Mola wao.

 Na wapo Waislamu wenye maradhi ya kutoufuata Uislamu kama unavyotakiwa, baadhi yao utawaona kuwa wanachaguwa yenye maslaha ya kidunia kuyafuata na kuyatilia mkazo, na yenye kuzuia raha na matamanio ya kimaisha hupingwa na kutofuatwa. Na matokeo yake ni imani hutoweka, maasi huzidi,  na upotofu unapata nguvu na umma unaagamia.

 Ikiwa kupinga amri za viumbe wenzetu ni makosa na tunaogopa, vipi leo tunampinga yule ambaye ametuumba, ametuleta duniani na kuturuzuku kwa neema na rehma za kila namna, na ambaye anatulea na mwishowe marejeo yetu yatakuwa kwake na tutahisabiwa kwa yote tuliyoyafanya, ikiwa mazuri au mabaya. Kwa hivyo tutasema nini tutakapo simamishwa mbele ya haki? Tutasema hatujui, hatukufundishwa au tumeghafilika? Sababu zote hizo hazikubaliki.

 Jukumu la kuamrishana mema na kukatazana mabaya.

Waliojisalimisha nafsi zao kwa Mwenyeezi Mungu (Waumini) huongozana na huamrisha mema an hukataza maovu. Huu ni wajibu na ni jukumu la kila mmoja wetu kutumia njia zozote zile zinazoweza kutumika ili kuweza kuufikisha ujumbe na kufikia lengo la kuunyanyuwa Uislamu kwa kuilimishana na kukataza maovu, na kujiadilisha katika kutii amri za Mola wetu.

 Kwani Mwenyeezi Mungu kishatuahidi na keshaandaa Pepo nzuri zenye mabustani yenye kupita mito ndani yake kwa wale waja wake wema, waliofuata aliyowaamrisha na wakaacha waliokatazwa.

æóÇáúãõÄúãöäõæäó æóÇáúãõÄúãöäóÇÊõ ÈóÚúÖõåõãú ÃóæúáöíóÇÁ ÈóÚúÖò íóÃúãõÑõæäó ÈöÇáúãóÚúÑõæÝö æóíóäúåóæúäó Úóäö ÇáúãõäßóÑö æóíõÞöíãõæäó ÇáÕøóáÇóÉó æóíõÄúÊõæäó ÇáÒøóßóÇÉó æóíõØöíÚõæäó Çááøåó æóÑóÓõæáóåõ ÃõæúáóÜÆößó ÓóíóÑúÍóãõåõãõ Çááøåõ Åöäøó Çááøåó ÚóÒöíÒñ Íóßöíãñ æóÚóÏó Çááøåõ ÇáúãõÄúãöäöíäó æóÇáúãõÄúãöäóÇÊö ÌóäøóÇÊò ÊóÌúÑöí ãöä ÊóÍúÊöåóÇ ÇáÃóäúåóÇÑõ ÎóÇáöÏöíäó ÝöíåóÇ æóãóÓóÇßöäó ØóíøöÈóÉð Ýöí ÌóäøóÇÊö ÚóÏúäò æóÑöÖúæóÇäñ ãøöäó Çááøåö ÃóßúÈóÑõ Ðóáößó åõæó ÇáúÝóæúÒõ ÇáúÚóÙöíãõ

 Na Waumini wanaume na Waumini wanawake wao kwa wao ni marafiki walinzi. Huamrisha mema na hukataza maovu, na hushika salaa na hutoa zakaa, na kumtii Mwenyeezi Mungu na Mtume wake. Hao Mwenyeezi Mungu atawarehemu. Mwenyeezi Mungu amewaahidi Waumini wanaume na Waumini wanawake Bustani zipitazo mito, wadume humo. Na makaazi mema katika bustani za kudumu, na radhi za Mwenyeezi Mungu ndio kubwa kuliko yote. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

At Tawba-71-72

 Maelezo zaidi

Aya mbili za juu zinatuelezea kuhusu tabia nzuri za waumini wanavyo katazana mabaya na kuamrishana mema, ambao vile vile wanasimamisha Salaa na kutoa Zakaa, na wanamtii Mwenyeezi Mungu na Mjumbe wake.

 Mwenyeezi Mungu amechukua ahadi kwa viumbe vyake kuwalipa rehma na kuwapa Pepo yenye mabustani mema, na makaazi mazuri ya kudumu, yenye kila aina ya raha na furaha.

 Tukizingatia kuhusu nguzo tano za Uislamu, tutaona kuwa Salaa na Zakaa ndizo mguzo zilizotajwa zaidi katika Qur’ani kwa mifano na mafahamisho, na vile vile Wajumbe na Mitume waliopita waliamrishwa ibada hizi kuzisimamisha na kuzitimiliza.

 Hapa tunapata dalili ya umuhimu wa nguzo hizi, kwa wingi wa thawabu zake na kuwa ni sababu kubwa ya uwongofu mzuri kwa Waislamu na utengezaji wa imani zao na hali ya maisha yao, iwapo nguzo hizi zitatimizwa kwa ukweli, kwa ikhlasi na kwa unyenyekevu.

 Tukiangalia njia kubwa ya kuchuma thawabu ni Salaa, kwani kila siku tunasimamisha salaa tano za faridha (zilizotulazimu), mbali salaa za sunna (nyengeza au ziada). Kwa hivyo hii ndio njia kubwa ya kujipatia thawabu kwa kumtakasa na kumuomba Mola wetu katika kila siku.

 Zakaa ndio njia ya pekee ya kuunyanyua umma wa Kiislamu, na ndio njia ya kujipatia thawabu za kuendelea kwa kutukuza wito wa Mola wetu na kuleta mapenzi na mahusiano mema kwa viumbe waliojisalimisha nafsi zao kwa Mola wao mtukufu ‘Allah’.

 Nini maana ya Uislamu?.

Uislamu ni masalimisho ya nafsi kwa kumkubali Mungu mmoja tu wa haki (Mwenyeezi Mungu) na kufuata kanuni, nidhamu na sharia zake zilizokamilika na zisizokuwa na shaka wala zisizohitajia kubadilishwa kwa kuongezwa au kupunguzwa katika zama zote.

 Sharia hizo tumeletewa sisi viumbe zituongoze na kutuelekeza katika njia ya uwongofu, ili tupate amani kamili ya kiwiliwili na akili kwa kujisalimisha nafsi zetu kwa Muumbaji mmoja tu wa kweli ‘Allah’ kwa madhumuni ya kupata amani na raha za duniani na Akhera.

 Kwani mafanikio mema hayo ya uwongofu ya duaniani ndio yatakaotupelekea na kutuongoza katika njia ya kupata kulipwa na Mola wetu Pepo, Mabustani yenye kila aina ya raha za maisha, huko kila tutakachokitamani tutakipata, hakuna kuumwa wala kufa, hakuna shida wala taabu, ni raha za kudumu za kuendelea moja kwa moja.

 Sharia hizo zitokazo kwa Mwenyeezi Mungu zimetufikia kwa kupitia kwa wajumbe wake. Kazileta kwa ajili ya kuwatoa viumbe vyake kutoka katika upotovu na giza la ujinga na kuwaonesha mwangaza wa njia ya uwongofu. Mwenyeezi Mungu hawezi kuleta Sharia zake kwetu moja kwa moja, bali hutumia wajumbe wake (Malaika) kama Jibril ambaye huufikisha ujumbe huo kwa Mtume wake, naye huwafikishia viumbe ujumbe huo na kuufahamisha na kuuelekeza ili uweze kufahamika na kufuatwa.

 Kanuni na sharia hizo hazikuletwa mara moja, yaani Qur’ani haikuteremshwa yote mara mmoja, bali imeteremshwa kidogo kidogo kwa mujibu wa wakati wake na sababu zake mpaka ikakamilika kwa muda wa miaka 23. Halafu akatuachia viumbe vyake tuzifuate sharia hizo na kutuelekeza na kutupa mifano mbali mbali kwa kutueleza nini raha za peponi kwa watakaofuata sharia zake, na nini adhabu za motoni alizoziweka kwa waje wake watakaomuasi katika amri zake.

 Sasa tukizifuata hizi kanuni na sharia alizotuletea Mola wetu tutafanikiwa hapa duniani, na mafanikio makubwa zaidi ya milele (ya kudumu) yatakuwa huko akhera. Sasa tukimuasi Mola wetu kwa kutozifuata hizo kanuni alizotuletea; basi huenda tukaanza kuadhibishwa hapa hapa duniani, na adhabu kali zaidi zisizoweza kupigiwa mfano zitawakuta wapotofu siku ya Akhera kwa wale waliokataa kufuata dini ya Mwenyeezi Mungu.

 Jina la Uislamu ni tafauti kabisa na majina yanaotumika kwa kutaja dini nyangine zilizopita ambazo majina yake yamebadilishwa na wafuasi wake na kutumika kwa jina au muasisi wake au kabila au nchi wanayoishi kama vile mfano Ukristo unatokana na Christ (Yesu), Buddism unatokana Budda. Hinduism inatokana nchi au ardhi wanayoishi hao wafuasi, na Judaism inatokana na jina la kabila judi. Lakini jina la Uislamu linatokana na amani na salama kwa kujisalimisha kwa Mungu mmoja wa haki.

 Ijapokuwa wamejaribu kuita Uislamu kwa jina la Muhammadanism, ili waulinganishe na Christianity au Buddism, lakini hawakufaulu kwani Muhammad ni Mjumbe tu, sio yeye muasisi wa Uislamu. Uislamu ni dini ya Mwenyeezi Mungu na ni makosa kutumia jina hilo kwa kuita Uislamu au wafuasi wa dini ya Uislamu.

 Jee! Uislamu una mfumo wa pekee?

Bila shaka Uislamu una mfumo na nidhamu  tafauti na nidhamu nyangine zote za kidunia zikiwa za kidini, kisirikali, za kisiasa za kisayansi, za kihistoria au za kibiashara. Na tafauti ya kwanza ni kuwa nidhamu za Kiislamu  zimepeya na ziko hai, na wala hazihitaji kubadilishwa cho chote si herufu, si aya wala si sura. Kila zama zikipita nuru yake inachomoza zaidi na kukubalika na kufahamika kwa uwazi zaidi.

 Kitu cha pili kuwa nidhamu ya Uislamu inatumia katika Qur’ani mifano ya maelekezo ya waliopita au vitendo vilivyopita, au matokeo na malipo ya wafanyao mazuri (Pepo) na malipo ya wafanyao mabaya (moto) na kumfanya mtu afikiri na kutumia akili yake kwa kuyakubali kwa uhuru wa nafsi yake, kutokana na imani yake bila ya kushawishiwa au kulazimishwa kuamini kuwepo kwa Mungu mmoja tu ‘Allah’

 Jambo la tatu ni kuwa Uislamu unaridhisha akili ya viumbe kwa kuwafundisha na kuwasomesha na kuwashajiisha kutafuta elimu ziada kwa kuwapa au kutaja mifano katika Qur’ani ya mambo ya ilimu ya sayansi, ilimu ya anga, ilimu ya maubile ya vitu na mengineyo. Uislamu haukuweka vizingiti kwa kusema ukichunguwa mambo ya anga au bahari utakufuru au kumshirikisha Mwenyeezi Mungu, bali watu wanashajiishwa kutafuta ilimu ili wazidi kujua kuwepo kwa Muumbaji.

 Jambo la nne ni kuwa Uislamu hautuzuilii au kutuwekea vikwazo katika mambo ya kidunia, kama idadi ya kuowa, uwezo wa kumiliki mali, kuwa na nyumba nzuri, kula chakula kizuri, bali imetuwekea mipaka, ulinzi na nidhamu kwa ajili ya maslaha ya nafsi pamoja na jamii yote.

 Jambo la tano ni Uislamu haumuongozi mtu au jamii peke yake, bali uwongozi wake ni wa ulimwengu wote kwa jumla. Hautufundishi kujishughulikia nafsi zetu tu bali unatuongoza kuwa wasaidizi na wema kwa watu wote na kuwapa haki zao wote waliotuzunguka, wazee, ndugu, watoto, mke, mume, jirani na hata mpita njia.

 Nini maana ya Muislamu?.

Muislamu ni yule kiyumbe aliyejisalimisha nafsi yake kwa Mwenyeezi Mungu (Muumba wa ulimwengu na vilivyokuwemo ndani yake) kwa kufuata aliyoamrishwa na kuwacha aliyokatazwa.

 Kujisalimisha ni kuwa cho chote unachokitenda basi unakitenda kwa ajili ya Mola wako, yaani unakifanya kwa kutarajia thawabu. Na jambo lolote linalokukabili katika mitihani ya kidunia, ama likiwa  zuri basi wajibu wako ushukuru, na ikiwa unalifikiria kuwa baya basi wajibu wako ustahamili na Mungu wako umdhukuru. (umkumbuke) Mwenyeezi Mungu anajua kila kitu mja wake anachokifanya, kikiwa cha siri au cha dhahiri. Kwa hivyo kila kiumbe ana hisabu yake ya mazuri na mabaya anayoyafanya.

 Utukufu wa kiumbe huyo aliyejisalimisha nafsi yake kwa Mola wake, unatokana na uchamungu wake, hautokani na rangi yake, kabila yake, uwananchi wake, utajiri wake, uzuri wake au cheo chake.

Åöäøó ÃóßúÑóãóßõãú ÚöäÏó Çááøóåö ÃóÊúÞóÇßõãú Åöäøó Çááøóåó Úóáöíãñ ÎóÈöíÑñ

Mwenyeezi Mungu anasema: “Hakika aliyemtukufu (bora) kati yenu kwa Mwenyeezi Mungu ni huyo aliye mcha mungu zaidi katika nyinyi. Hakika Mwenyeezi Mungu ni mwenye kujua (kila kitu), mwenye (ujuzi) khabari ”.

Al Hujuraat-13

 Kiumbe yupi aliye bora?

Kwa hivyo ikiwa una uzuri wa sura au umbo, nguvu, cheo kikubwa, tajiri mkubwa na mengineyo yote, na sifa zote za kidunia, lakini jua na ufahamu kuwa mbele ya Mwenyeezi Mungu sifa zote hizo hazina kima (thamani). Aliye bora na mtukufu ni yule mcha mungu anayefuata yote aliyoamrishwa na anayeacha yote aliyokatazwa na Mola wake. Hakuna maneno zaidi ya haya, wala hakuna kuzungushana kwani kila kitu kipo wazi kabisa.

 Nini maana ya kafiri?.

Kafiri ni yule kiumbe aliyejitoa katika himaya ya Mwenyeezi Mungu, au akakataa kuamini na kufuata sharia na kanuni za Mola wake. Akapinga aliyoamrishwa, na akafanya aliyokatazwa na akawacha alioamrishwa.

Mwenyeezi Mungu ni Mungu wa viumbe vyote.

Tumeeleza mwanzo kuwa Mwenyeezi Mungu ndiye aliyeteremsha Mitume (Wajumbe) na ndiye aliyeleta vitabu vya kufuatwa na viumbe vyake kwa madhumuni ya kuwaongowa katika njia ya haki. Bila ya kuwa na sharia ya Mwenyeezi Mungu na kuifuata, basi viumbe tutakuwa tunaishi maisha ya kinyama, yenye kila aina ya mazonge na dhiki za kimaisha.

 ÞõæáõæÇú ÂãóäøóÇ ÈöÇááøåö æóãó ÃõäÒöáó ÅöáóíúäóÇ æóãóÇ ÃõäÒöáó Åöáóì ÅöÈúÑóÇåöíãó æóÅöÓúãóÇÚöíáó æóÅöÓúÍóÞó æóíóÚúÞõæÈó æóÇáÃÓúÈóÇØö æóãóÇ ÃõæÊöíó ãõæÓóì æóÚöíÓóì æóãóÇ ÃõæÊöíó ÇáäøóÈöíøõæäó ãöä ÑøóÈøöåöãú áÇó äõÝóÑøöÞõ Èóíúäó ÃóÍóÏò ãøöäúåõãú æóäóÍúäõ áóåõ ãõÓúáöãõæäó

Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyeezi Mungu na yale tulioteremshiwa sisi, na yalioteremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is’hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyopewa Musa na Isa, na pia waliyopewa Watume wengine kutoka kwa Mola wao, hatutafautishi baina ya yoyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.

Al Baqara-136

 Maelezo zaidi

Hapa wanaambiwa waliojisalimisha kwa Mola wao (Waislamu) kuwa waambie wale Mayahudi na manasara wanaokataa kumfuata Muhammad kwa alioletewa, kuwa sisi tunamuamini Mwenyeezi Mungu na yale tulioteremshiwa kwa watume waliopita. Na wala hatutafautishi yoyote kati ya Mitume hao, na sisi tumemkubali Muhammad na tumesilimu.

 Vitabu vya Mwenyeezi Mungu alivyoviteremsha.

Jumla ya vitabu vyote vilivyoteremshwa na Mwenyeezi Mungu kwa ajili ya uwongofu wa waja wake kupitia kwa Wajumbe wake ni Mia moja na nne (104) kama hivi ifuatavyo:

 Vitabu 50 kwa Mtume Shaith (as)

Vitabu 30 kwa Mtume Idriis (as)

Vitabu 10 kwa Mtume Ibrahim (as) (Vitabu-Suhuf)

Vitabu 10 kwa Mtume Musa (as) (Suhuf kabla ya Taurat)

Kitabu   1 kwa Mtume Musa (as) Taurat

Kitabu   1 kwa Mtume Daud (as) Zabur

Kitabu   1 kwa Mtume Issa (as) Injiil

Kitabu   1 kwa Mtume Muhammad (SAW) Qur’ani

 Watume waliotajwa katika Qur’ani (ishirini na tano)

1-Adam       2-Idris         3-Nuuh        4-Huud        5-Saleh       

6-Ibrahim     7-Luut         8-Ismail       9-Is’haak     10-Yaakub  

11-Yusuf     12-Shuayb   13-Ayyub    14-Dhul-kifl  15-Mussa

16-Harun     17-Daud      18-Suleiman 19-Ilyas       20-Ilyasaa

21-Yunus     22-Zakaria    23-Yahya     24-Issa        25-Muhammad

 Kwanini kukawa na Mitume na vitabu zaidi ya kimoja?

Mwenyeezi Mungu kateremsha ujumbe katika zama mbali mbali na katika miji mbali mbali, na uteremshaji uliendelea mpaka kufikia Mitume hii ya mwishoni kama Mtume Musa, Mtume Issa na Mtume Muhammad.

 Sababu kubwa ya kuteremshwa Mitume baada ya Mitume ni kuwa baada ya kupita miaka mingi na kufa hii Mitume, yale yalioteremshwa yanakuwa hayafuatwi tena na viumbe. Na kila miaka ikipita upotofu unakuwa unazidi kupata nguvu. Kwa hivyo Mwenyeezi Mungu huleta Mjumbe mpya, na Ujumbe mwengine kwa ajili ya kuwaokowa na kuwaongoza viumbe ili wafuate njia ya haki.

 Sasa tukitazama alipokuja Mtume Issa, ilikuwa viumbe wote waikubali na kuifuata dini hii mpya, yaani mpaka Mayahudi waache kufuata Taurati na wafuate Injiil, kwani kwa wakati ule ndio dini iliofuatia na imekuja na maamrisho mapya. Na vile vile ilivyokuja Qur’ani ilikuwa wajibu dini za nyuma ziwachwe na dini hii ya Uislamu ifuatwe na viumbe wote. Kwa kuwa Mungu aliyeteremsha Zabur, Taurati, Injili na Qur’ani ni yule yule.

 Kama tulivyoeleza mwanzo, kutokana na maslaha ya kidunia ya viongozi wa dini hizo, huyakataa haya na kuhakikisha wafuasi wao wapo pamoja nao, ili vyeo vyao na mapato yao yaweze kuendelea. Hata kufikia hadi kubadilisha maelekezo ya Mola wao, na kuandika wanavyotaka wao, na kufuata mila na utamaduni wao, badala ya kufuata maelekezo na maamrisho walioletewa na Mola wao.

 Huu ni upotofu mkubwa, na haya ni makosa makubwa ya kupinga maamrisho ya haki, na kufuata matamanio ya nafsi. Tunamuomba Mola wetu awazidue na kuwaongoza waliopotea uwajie muangaza na kuweza kuona nuru ya njia ya haki waifuate na kuwa katika himaya ya Mwenyeezi Mungu duniani na Akhera, Amiin.

 Viumbe tumepewa uhuru wa kufikiri na kuzingatia, kwa hivyo tuitumie hiyo akili kwa kujiuliza nafsi zetu kuwa ikiwa mfano kuna mtungaji wa kitabu anayesifika sana, ambaye kitabu chake hicho huwa anakisawazisha kila baada ya miaka fulani na kuchapisha chapa mpya. Sasa ikiwa mtu anataka kununua kitabu hicho, jee! Atanunua chapa za zamani au atanunua kitabu kilicho chapishwa karibuni? Sote tutanunua chapa mpya kwa sababu itakuwa bora kuliko chapa za zamani.

 Sasa tukirejea tena Mungu anayeabudiwa ni yule yule mmoja kwa wote, na vitabu alivyoviteremsha kwa waja wake ni yeye ndiye aliyevileta kwa madhumini ya kuwaongowa viumbe vyake, kwa hivyo kitabu cha kufuatwa na viumbe vyote ni kitabu cha mwisho (Qur’ani) ambacho kimechukuwa yaliokuwamo katika vitabu vyote vilivyopita.

 Tunajua kuwa Qur’ani ni kitabu cha mwisho, na wala hakuna kuja kwa Mtume mwengine mpya, wala kuja kwa kitabu kipya. Lakini lau kama tumeletewa na Mola wetu Mjumbe (Mtume) mpya na uwongozi mpya, basi ingelikuwa tuwache vitabu vya Mungu vyote vilivyopita pamoja na Qur’ani na tufuate kitabu chenye maamrisho mapya.

 Hili ni jambo liko wazi, na linaingia akilini na kukubalika kwa kila aliyekuwa anataka haki na ukweli, na anayeipenda nafsi yake kwa kuamini kuwepo kwa Mungu mmoja, kwa hoja zote zilizowazi kabisa.

 Ndugu msomaji, ikiwa wewe bado hujajisalimisha kwa Mola wako, basi sikwambii silimu, lakini nakuomba usome zaidi na ujaribu kuuliza watu wenye kufahamu dini uzuri zaidi, ili upate maelekezo mazuri na ya kweli mpaka ukinai nafsi yako, na ujuwe cho chote unachokifanya, unakifanya kwa sababu gani. Asikwambie mtu fuata tu, kwani kila ukijua sababu ndio utafahamu zaidi na utayatekeleza kwa imani ya kweli.

 Uislamu hakuna kuvungana kwa maneno, yote yanayofuatwa yana maelekezo na yana sababu na misingi maalumu kwa nini yanafanywa. Na akikwambia mtu fanya tu kama wanavyofanya wengine, basi jua yeye huyo haifahamu dini yake uzuri, na tafuta mtu mwenye kufahamu akupe maelekezo zaidi.

 Kiumbe akizaliwa na kuja duniani, anakuja katika hali ya kuwa yuko huru, lakini akifika duniani anakumbana na mazonge ya kila namna ambayo yanampelekea kupotea ikiwa hakupata maelekezo mema. Na upotofu huo unatokana na mazingira aliyoinukia au anayoishi nayo.

 Kutokana na maendeleo ya kidunia ambayo yanatumika vibaya kwa kukusudia katika vyombo vya habari na mafundisho ya elimu na mambo mbali mbali ya kimaisha, mara nyingi tunajikuta tumetekwa kiakili, kimawazo na kimaisha na kuelekezwa katika njia ya upotofu na kuambiwa kuwa haya ndio maendeleo na ndio njia ya pekee ya raha na mafanikio ya maisha.

 Njia pekee ya uwongofu katika maisha ya kiumbe ni kushikamana na maamrisho ya dini ya haki, yanayotokana na Mungu wa haki anayestahiki peke yake kuabudiwa na kutegemewa na viumbe vyake vyote. Na kwa lolote jengine tunalolifanya la kimaisha tunatakiwa tuliambatanishe na kulilinganisha na maelekezo kutoka kwa Mwenyeezi Mungu.

Kwa nini wakaumbwa Malaika, Binaadamu na Majini?

Mwenyeezi Mungu kaumba malaika ambao si katika jinsi ya Binaadamu wala Majini. Viumbe hawa hawamuasi Mola wao kwa wanayoamrishwa, wao hawali wala hawanywi, wala hawana sifa za uke (usichana)wala sifa za uume (uvulana). Wameumbwa kwa ajili ya kuabudu na kutekeleza amri za Mola wao.

 Binaadaamu na majini wameumbwa vile vile kwa ajili ya kumuabudu Mwenyeezi Mungu mmoja, hatukuletwa duniani kwa ajili ya kuja kutafuta mali, utawala na raha za kidunia. Mambo ya kidunia yote unaruhusiwa kuwa nayo na kumiliki kila unachoweza kuwanacho katika sharia na mipaka yake. Lakini ibada ndio msingi na madhumuni ya kuletwa duniani.

 Kwa hivyo kiakili ikiwa tumeumbwa na kuletwa duniani ili kwa ajili ya kumuabudu Mwenyeezi Mungu, basi tunavyotakiwa katika masaa 24 ya kila siku inatuwajibikia kuyatumia zaidi ya nusu ya masaa hayo katika kufanya ibada.

 Ndio maana Mola wetu alituamrisha kwanza kusali salaa 50 katika kila siku moja, halafu tukapunguziwa na kupunguziwa mpaka zikafika salaa 5 tu. Lakini malipo ya salaa hizo tano tunalipwa sawa na salaa 50 kwa rehma na kwa mapenzi ya Mola wetu. Hii ndio dalili ya kuwa Mola wetu katuumba na kutuleta duani ili tuje kumuabudu. Na ibada sio salaa tu, kuna kufunga, kuna kuhiji, kuna kutowa zakaa na mengineyo.

 Sasa hebu tufikirini kama ndio ingekuwa tumeachiwa na zile salaa 50 kuzisali kila siku, basi kwa uchache tungelikuwa tunasali salaa 2 katika kila saa mmoja si usiku si mchana. Sasa kungelikuwa na uwezo wa kuendelea kulala masaa 8 mfululizo na kufanya kazi masaa 8, na kupumzika masaa 8 katika siku mmoja ya masaa 24? Wengi wetu tungeshindwa kuyatimiza kama yanavyotakiwa. Tumeamrishwa salaa 5 na bado kuna watu wanashindwa kuzitimiza, ewe kiumbe unataka nini zaidi ufanyiwe?

 Kwa hivyo ibada hapa inakusanya mambo yote ya kheri ikiwa kusali, kutafuta rizki ya halali, kufunga, kuhiji, kutoa zaka, kumdhukuru (kumtaja) Mola wako, kusomesha na kuelimisha wenzio, kuupigania Uislamu kwa hali na mali na mengineyo yote ya kheri basi ni ibada. 

æóãóÇ ÎóáóÞúÊõ ÇáúÌöäøó æóÇáúÅöäÓó ÅöáøóÇ áöíóÚúÈõÏõæäö  ãóÇ ÃõÑöíÏõ ãöäúåõã ãøöä ÑøöÒúÞò æóãóÇ ÃõÑöíÏõ Ãóä íõØúÚöãõæäö  Åöäøó Çááøóåó åõæó ÇáÑøóÒøóÇÞõ Ðõæ ÇáúÞõæøóÉö ÇáúãóÊöíäõ

Nami sikuwaumba Majini na Watu ila (isipokuwa) waniabudu mimi. Na sitaki kwao rizki, wala sitaki wanilishe. Hakika Mwenyeezi Mungu ndiye mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu madhubuti.

Adh-dhaariyaat-56-58

 Maelezo zaidi

Hapa tukizingatia tutaona kuwa Mwenyeezi Mungu hakutuumba ila kwa ajili ya kumuabudu. Na tukimuabudu basi yeye hanufaiki na kitu, tunamuabudu ili sisi tupate faida na manufaa kutoka kwake kwa kutulipa aliyotuahidi viumbe vyake.

 Kwa hivyo Mwenyeezi Mungu hataki kitu cho chote kwetu wala si muhitaji wa jambo lo lote, bali anataka tumuabudu kwa kuwa yeye ndiye mwenye kutulisha, kuturuzuku, kutuhami na kutuongoza. Na anataka  tuchume thawabu wenyewe kutokana na mambo ya kheri aliyotuamrisha ili atupe Pepo aliyotuahidi viumbe vyake.

 Sasa kama tunavyojua kuwa Binaadamu na Majini wameumbwa kwa ajili ya kumuabudu Mwenyeezi Mungu. Na hilo ndio lengo la Mola wetu, kwa hivyo  jee! ndugu zangu tunalitimiza lengo hilo? Na ikiwa hatukulitimiza na kulikamilisha, basi tujuwe kuwa kuna moto mkali wa jahannam unatungojea. Ni wajibu kufikiri kwa makadirio ya moto wa duniani (tunaoutumia) ukitupata kidogo tunaruka na kupaparika, roho mbichi inataka kututoka. Jee! Moto huo ambao umefanywa khasa kwa ajili ya kuwatesa waasi, ukali wake utakuwa hali gani?

Muandishi: Ali S. Al Harrassy ©   asharasy@omantel.net.om

 

Copyright ©2004  Uislam.net