Waalaykum Salaam warahmatu-LLahi wabarakaatuh
Jawabu:
Kwa mujibu wa wenye ilmu, utumiaji wa maji ya kisima kilichomo/kilichochimbwa katika shamba lilonyan'ganywa si haramu kwa asiyechukua/asiyenyan'ganya ardhi hiyo; kwani maji ya kisima hayamilikiwi na mtu; bali mwenye kisima anamiliki shimo lenyewe tu likiwa katika ardhi yake.
Dalili ya hayo ni kauli ya Mtume -rehma za Allah na amani zimshukie- "Waislamu ni washirika katika matatu: maji, nyasi, na moto"; imepokewa na Abu Daud, Ahmad, Ibnu Majah na wengine. Wa'LLahu A'lam.
Abukhalil.
|