ukumbi  

Go Back   ukumbi > ukumbi Main Category > UKUMBI WA MASUALA ya DINI > Masuala mengineyo

 

 

LinkBack Thread Tools
  #1 (permalink)  
Old 10-06-08,
Junion Member
 
Join Date: 09-02-05
Location: Oman
Posts: 114
Default Dada anauliza hivi

Assalama Alaykum WarahmatuLlahi Wabarakaatuh,

Dada zetu wanauliza hivi,

1. Jee kukata kucha wakati wako katika siku zao za mwezi haijuzu?

2. Jee ikiwa wakati huu huu akichana nywele na zile ambazo zinotoka katika kitana ati ni lazima aziweke mpaka amalize siku zake halafu azitoharishe ndio azitupe. Haya makubwa kwangu.

Hata kucha ati wazitoharishe kwanza halafu wazitupe.

Tutoeni ujahili.
  #2 (permalink)  
Old 15-06-08,
Abukhalil's Avatar
Msimamizi wa Masuala ya Dini
 
Join Date: 07-09-04
Posts: 1,202
Default

Waalaykumussalaam warahmatu-LLahi wabarakaatuh

Jawabu:

Hayo hayana asli katika Sharia -kwa mujibu wa wenye ilmu- hata kama yametajwa katika baadhi ya vitabu; bali kukata kucha ni katika unadhifu unaotakiwa kisharia.

Kisha mwanamke hujitoharisha kwa ibada si kwa kuwa alikuwa najis, na kwa hiyo hapaswi kuosha ila kilicho mwilini mwake.

Hata hivo nywele za mwanamke ni aura (yaani sehemu inayopaswa istiriwe isionekane na wasio mahramu); hata zikitoka inapasa azikusanye na kuzifukia au kuzificha katika katika kitu kama karatasi au mfuko nk kabla kuzitupa jaani.
Wa'LLahu A'lam.

Abukhalil.
 

Bookmarks


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)

 
Thread Tools

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are On
Pingbacks are On
Refbacks are On



All times are GMT +5. The time now is .


Powered by vBulletin Version 3.8.3
Copyright ©2000 - 2010, Jelsoft Enterprises Ltd - Upgraded by SurCity.net.