Waalaykum Salam warahmatu-LLahi wabarakaatuh
Jawabu:
Naam, bila shaka kuchinja siku ya mwanzo kuna ubora na fadhila zaidi kuliko siku ya pili; kadhalika siku ya pili ni bora kuliko ya tatu, n.k.; kwani kuchinja wakati wa mwanzo ni katika kukimbilia mambo ya kheri, ambako kuna fadhila zaidi, kama ilivo kwa sala na ibada nyenginezo. Wa'LLahu A'lam.
Abukhalil.
|