Wapi Utakwenda siku ya Eid??
Assalam Aleykum Warahmatullahi Wabarakatuhu.
Ndugu zangu waislamu, mwezi wa Ramadhani umekaribia kutuaga, na watu wameshughulika katika kutafuta na kutayarisha vitu vizuri vya eid, ikiwa ni vyakula au mavazi...
Moja katika jambo zuri siku ya Eid ni ule mkusanyiko wa familia katika sehemu moja, wanapokutana jamaa na ndungu wakaulizana hali na kujuliana habari zao, hii ni neema kubwa anapaswa Allah kushukuriwa.
Kwa hivyo kama utakuwa na safari na marafiki zako, bora siku ya kwanza icheleweshe, ili upate nafasi ya kukaa na familia na jamaa na waliokaribu, kwani nafasi kama hizi si aghlabu kujumuika pamoja ila katika minasaba ya eid. Tunawatakia Waislamu mafanikio mema na umoja, na aliye mbali na familia na wazee wake, basi hata kama atakuwa na marafiki milioni hatakuwa si mwema kwako. Wa kufanyiwa wema kwanza ni wazazi na jamaa kabla ya wengine.
shukarn
uislam
|