Waalaykum Salaam warahmatu-LLahi wabarakaatuh
Jawabu:
Nadhani unakusudia saumu ya "Siku ya Arafa", ambapo mahujaji huwa katika kisimamo cha Arafa. Imethibiti kuwa Mtume wa Allah -rehma za Allah na amani zimshukie- hakufunga siku hiyo alipohiji. Kwa ajili hiyo, imefahamika kuwa himizo lake -rehma za Allah na amani zimshukie- la kuifunga siku hiyo ni kwa wale wasiokuwa katika hijja.
Wenye ilmu wamesema kuwa hikma ya kuto kufunga siku hiyo kwa mwenye kuhiji ni kumfanya awe na nguvu na hamasa ya kumdhukuru Allah kwa wingi na kumuomba tangu adhuhuri hadi magharibi bila ya kudhoofika.
Halikadhalika sala ya eid haikusuniwa kwa mahujaji kwasababu wakati wa sala hiyo wao huwa wameshughulika na kupiga jamra la 'Aqaba, na wakimaliza hufanya ibada nyenginezo za hijja kama kuchinja, kunyoa na kutufu tawafu ya ifadha.
Wa'LLahu A'lam.
Abukhalil.
|