ukumbi  

Go Back   ukumbi > ukumbi Main Category > UKUMBI WA MASUALA ya DINI

Reply

 

LinkBack Thread Tools
  #1 (permalink)  
Old 13-02-10,
New Member
 
Join Date: 07-11-09
Posts: 2
Default Kuamkia kwa mkono (mikono)

Salaam Alaikum,

Suala langu ni kuhusu kuamkiana kwa mikono baina ya mwanaume na mwanamke.
Jee ipo ruhusa ya kumuamkia kwa mkono mke wa:
1. Ammi yako
2. Mjomba yako

Shukraan.
Reply With Quote
  #2 (permalink)  
Old 21-02-10,
Abukhalil's Avatar
Msimamizi wa Masuala ya Dini
 
Join Date: 07-09-04
Posts: 1,202
Default

Waalaykum Salaam warahmatu-LLahi wabarakaatuh

Jawabu:

Rukhsa ipo wakiwa wamefikia umri wa uzeeni, na kuepuka ni aula; vinginevo haijuzu. Wa'LLahu A'lam.

Abukhalil.
Reply With Quote
  #3 (permalink)  
Old 20-03-10,
Junion Member
 
Join Date: 05-11-04
Location: South Maabela
Posts: 62
Send a message via MSN to Sami Send a message via Skype™ to Sami
Default

Sheikh

Asallam alaikum,

umri wa uzeeni ulioruhusiwa ni kuanzia miaka mingapi.
Reply With Quote
  #4 (permalink)  
Old 31-03-10,
Abukhalil's Avatar
Msimamizi wa Masuala ya Dini
 
Join Date: 07-09-04
Posts: 1,202
Default

Waalaykum Salam warahmatu-LLahi wabarakaatuh

Jawabu:

Sikuona katika wenye ilmu aliyeainisha umri huo kwa miaka, lakini wanasema siyo kusita kupata hedhi tu, bali na kufikia hali ya kuto kutamani kuolewa na kuto kutamaniwa na waume kwa utuuzima.

Hao ndio walioruhusiwa, katika surat A'Nuur aya 60, kupunguza nguo wanazovaa kwa stara ya nje; yaani wanaweza kuacha kuvaa abaya (baibui) wakatosheka na kanzu zao na mtandio bila kujipamba na kuonesha mapambo yao. Hata hivo wameambiwa wakijitakasa kwa kuto kuacha stara kamili ni bora kwao. Kutokana na rukhsa hiyo ndiyo kumekuwa na kauli inayoruhusu kupewa mikono lakini pia kuacha ni bora. Wa'LLahu A'lam.

Abukhalil.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)

 
Thread Tools

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are On
Pingbacks are On
Refbacks are On



All times are GMT +5. The time now is .


Powered by vBulletin Version 3.8.3
Copyright ©2000 - 2010, Jelsoft Enterprises Ltd - Upgraded by SurCity.net.