ukumbi  

Go Back   ukumbi > ukumbi Main Category > UKUMBI WA MASUALA ya DINI

Reply

 

LinkBack Thread Tools
  #1 (permalink)  
Old 18-07-10,
Active Member
 
Join Date: 11-10-04
Posts: 187
Default Kulipa ramadhani

Asalam aleykum warahmatulwa wa barakat sheikh..

Shekh mzee wetu anauliza.
No 1. Mwakajana hakufuga ramadhani kwajili ya maradhi na mpaka sasa hivi bado hawezi kufunga(hajalipa ramadhani yake) kuna watu wanamwambia angoje mwakani jee angoje au alishe masikini.
No 2. Kwa kila siku maskini wangapi na kiasigani atowe na jee anaweza kumpa msikini moja
Reply With Quote
  #2 (permalink)  
Old 01-08-10,
Abukhalil's Avatar
Msimamizi wa Masuala ya Dini
 
Join Date: 07-09-04
Posts: 1,202
Default

Waalaykum Salam warahmatu-LLahi wabarakaatuh

Jawabu:

Akiwa hataraji kupona maradhi yake akaweza kufunga baadae, anapaswa badala ya kufunga atoe fidia ya kulisha masikini mmoja kwa kila siku ya Ramadhani iliyopita na kadhalika itakapofika Ramadhani ijayo. Maskini apewe milo miwili kwa kila siku ya Ramadhani au nusu pishi ya mchele (= kilo moja na gramu 25). Akichukua rukhsa ya kutoa thamani aongeze kidogo kwa ajili ya usalama zaidi; mfano akitoa riali moja na nusu ya Omani inatosha kwa sasa. Maskini mmoja anatosha kupewa kwa siku zote.

Akiwa hana uhakika kama baadae ataweza au hataweza kufunga, ni bora akatoa fidia kwa mwaka uliopita madamu Ramadhani ya pili imeshafika naye bado hajaweza kufunga na ni mtu mzima, kisha akiweza baadae atalipa.

La kuzingatia ni kuwa fidia inapomlazimu humlazimu katika mali yake mwenyewe; akiwa hana mali anasameheka wala haiwalazimu wanawe ila wakipenda kumtolea kama sadaka.

Wa'LLahu A'lam.

Abukhalil.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)

 
Thread Tools

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are On
Pingbacks are On
Refbacks are On



All times are GMT +5. The time now is .


Powered by vBulletin Version 3.8.3
Copyright ©2000 - 2010, Jelsoft Enterprises Ltd - Upgraded by SurCity.net.