 |
MAONESHO YA HAJ KWA PICHA - KUTUMIA
POWER POINT
Endelea
|
Shukrani zote
zinamstahikia Allah aliyefaradhisha kuihiji Nyumba Yake Takatifu,
akaifanya hija mkutano mkuu wa kidunia wa Uislamu. Kisha rehema na
amani zimshukie Nuru ya uongofu, Taa ya gizani, aliyesema: “Pokeeni
kwangu ibada zenu za hija.”
Baada ya hayo:
Idara ya Muongozo wa
Wanawake imeona umuhimu wa kufasiri kwa Kiswahili kitabu
kilichotolewa na Kitengo cha Utafiti wa Kitaalamu katika Ofisi ya
Fatwa kiitwacho “HAADHA HUWA ALHAJJ”, yaani “HUKU NDIKO KUHIJI” ili
kuongeza manufaa yake kwa wasemao Kiswahili na kuwahudumia kati yao
mahujaji wa Nyumba ya Allah Takatifu katika upande wa muongozo na
maelekezo. Allah Ndiye wa kushukuriwa kwa mafanikio ya kutoka kwa
toleo hili la Kiswahili na Yeye, Aliyetukuka Ndiye tunayemuomba
anufaishe kwalo waja Wake.