|
|
HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA JUMUIYA |
1. Kufungua Madarasa ya kufundisha Qur - an
tukufu.
2. Kufundisha lugha ya kiarabu na nahau yake
pamoja na kusoma na kuandika kiarabu.
3. Kuzifanyia matengenezo misikiti mikongwe.
4. Kujenga miskiti mipya .
5. Kununua mabomba ya adhana na mashine zake.
6. Uchimbaji visima kwa ajili ya misikiti na
maeneo ya karibu.
7. Ujenzi wa shule ya kiislamu.
8. Kutoa misahafu na vitabu vya hadithi za
Mtume (S W A).
9. Kukusanya zakaa na kuzipeleka kwa wale
wanaostahiki (nao ni wengi).
10. Kutoa vitabu vya shule na nyenzo
nyenginezo.
11. Upatikanaji wa huduma za afya.
12. Kuanzisha mafunzo ya ushoni.
13. Kushiriki katika ujenzi wa nyumba kwa
familia maskini.
14. Kuozesha vijana wasiokuwa na uwezo wa
gharama za mahari na mahitaji yake.
15. Kuftarisha kwa wanaofunga mwezi wa
Ramadhani.
16. Kutoa mavazi kwa wanaohitaji wakati wa
sikukuu za iddi.
17. Kuwashughulikia watu wenye ulemavu.
18. Kutoa misaada na kutatua mahitaji ya hali
zote ya mayatima.
19. Kunyanyua na kuboresha hali ya maisha ya
familia maskini kwa kuanzisha miradi inayozalisha.
20. Kulipa madeni ya baadhi ya familiya
maskini.
21. Ununuzi wa magari kwa ajili ya kueneza
uislamu na kuwapatia wanafunzi usafiri wa kwenda na kurudi skuli n.k.
Jumuiya ya kiislamu ya kimataifa ya
Istiqaama inakukaribisha kwa njia zozote zinazowezekana kuunga mkono juhudi
zake kifedha au kimawazo kwa ajili ya kutimiza malengo yake thabiti katika
kueneza elimu na kuwasaidia waislamu duniani.
|