|
|
matembezi ya Samahat Sheikh Ahmed Al Khalili Mufti Mkuu wa Oman katika Maahad ya Istiqama -iliyoko Tunguu Zanzibar
|
يقول الله تعالى : (وما تقدموا لأنفسكم من خير تجدوه عند الله هو خيرا وأعظم أجرا واستغفروا الله إن الله غفور رحيم) ( Chochote katika wema unachokifanya kwa ajili ya nafsi yako, basi ujira (thawabu) wake mkubwa na zaidi utaukuta mbele ya Mwenyezi Mungu ). Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia rehma bwana Mtume ( S.A.W ) na kuwatakia radhi masahaba zake na kila mwenye kufuata mwendo wao mpaka siku ya mwisho. Amma Baad: Jumuiya ya Istiqama Inawakaribisha katika mtandao huu ulioundwa khususi kwa ajili ya kuwaelimisha Watukufu waislamu juhudi na huduma zote zinazotolewa na jumuiya. Fikra hii imekuja baada ya kuona ni vyema Waislamu wajue na wapate dalili kamili katika ile michango yao wanaypitowa kuwa haya mnayoyaona ndio matunda ya juhudi zenu, na kila mnachokitowa ikiwa mali au fiktra au ushauri, basi alhamdulilah mafanikio ni haya. Na vile vile hamasa ya kuwaomba waislamu waendelee na kazi hii tukufu itazidi baada ya kuziona juhudi hizi katika macho yao. Na jumuiya ya Istiqama iko tayari kujibu kila suala au kupokea kila ombi katika ukumbi huu. Na kazi hii ni yetu sote si ya Raisi ya Jumuiya na makamo wake, bali kila mmoja ni wajibu wake kuchangia kwa alichokuwa nacho.
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|
JUMUIYA YA ISTIQAMA Ndugu zangu Waislamu. Hizi ni baadhi ya picha zinazojieleza wenyewe kuhusu juhudi ya Jumuiya ya Istiqama katika sehemu mbali mbali Tanzania. Juhudi hizi husimama kwa misaada ya Waislamu pale wanapojitahidi kutoa mali zao. Ndugu zangu huduma nyingi hufaidika Waislamu wenzanu katika sehemu mbali mbali miongoni mwao mayatima. Miongoni mwa huduma hizo; kujenga misikiti na madrasa za kusomesha Quraan na kuchimba visima vya waqfu, pamoja na kulisha na kuvisha masikini, misada yote hii hupokelewa na Wahusika waliojitolea wakati wao katika kuutumikia uislamu na kuendesha mbele Juhudi za Jumuiya. Kwa kupata habari zaidi kuhusu Jumuiya ya Istiqama na maendeleo yake, pamoja na michango, tafadhali wasiliana ya Wahusika wa Jumuiya hii.
|
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|
|
Copyright © 2009 All right reserved for www.uislam.net |