CHUO CHA ISTIQAMA CHA MASOMO YA KIISLAMU - ZANZIBAR

 

Chuo cha Istiqaama cha Masomo ya Dini ya Kiislamu – Zanzibar ni taasisi ya taaluma ya mafunzo ya dini iliyo chini ya Jumuiya ya Kiislamu ya Istiqama ya Tanzania.

 

HISTORIA FUPI YA CHUO CHA ISTIQAMA:


Chuo cha Istiqama kimeasisiwa chini ya usimamizi wa Sk. Muhammed bin Salim Al Busaidi na Sk. Zahir bin Khalifa Al Alawi mwaka 1415H / 1995AD, kikafunguliwa awali katika Msikiti wa Istiqama wa Zanzibar, kikiwa na wanafunzi 32 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania, walimu 3 na afisa utawala 1.


Mwaka 1418H / 1998AD Chuo kilihamia kwa muda katika jengo la Madrasat Lemki ya watoto wa kike, na mwaka 1421H / 2001AD kikahamia katika makao yake ya kudumu iliyoko Tunguu kiasi kilomita 16 kutoka mjini Zanzibar, katika ardhi ambayo Tawi la Jumuiya ya Istiqama la Zanzibar lilijitolea kuinunua mahususi kwa ajili ya mradi wa Chuo cha Istiqama.



Chuo kilipohamia huko Tunguu, majengo yake hayakuwa zaidi ya msikiti, madarasa, dakhalia (makaazi ya wanafunzi) na nyumba mbili za wageni/walimu. Baadae ujenzi uliendelea likapatikana jengo la utawala na ofisi za walimu, jengo la maktaba, jengo la ukumbi wa kulia/mikutano/sherehe, nyumba za wapisi, na uwanja wa riadha.

 

AL - ISTIQAAMA AL - KHAIRIYA

A/C. NO : 03 - 513397 - 02

Oman International Bank (SAOG)

Mina Al- Fahal (MNF) - SULTANATE OF OMAN

 

 

Chuo cha Istiqama katika msikiti wa Istiqama wa Zanzibar

 

Chuo cha Istiqama katika jengo jipya na makao yake ya kudumu iliyoko Tunguu kiasi kilomita 16 kutoka mjini Zanzibar

 

MALENGO YA JUMLA YA CHUO CHA ISTIQAMA:
1. Kuinua kiwango cha elimu ya Dini ya Kiislamu   kwa vijana.
2. Kuipatia jamii walinganiaji wazuri wa Dini ya  Kiislamu.
3. Kutoa wahitimu waliohifadhi Qur-an tukufu, wenye   kuelewa  fiqhi na wajuzi wa sunnah za Mtume na maarifa  kamili ya itikadi sahihi ya dini, watakaoweza kusimamia  madrasa za kidini na shughuli nyenginezo za kheri.
4. Kutoa wahitimu wenye fani nyinginezo za elimu zitakazowasaidia katika maisha yao.
5. Kukuza uhusiano, udugu na upendano baina ya waislamu.

 

Moja katika Ofisi za Walimu

 

Darasa la ufundi wa Compyuta katika chuo cha Istiqama

 

MFUMO WA MASOMO KATIKA CHUO:
Ili kuipa umuhimu Lugha ya Kiarabu na kuzingatia ubora wa kusomea sharia ya Dini kwa lugha yake ya asili, Chuo cha Istiqama kimekuwa kikifuata mitaala ya vyuo viwili vinavyotambulika rasmi vilioko nchini Oman, baada ya kupata idhini kutoka vyuo hivyo; navyo ni:
1. Maahad Al-uluum Ash-shar-iyya.
2. Markaz Al-Sultan Qaboos lith –thaqafa Al-Islaamiyya.


TAKWIMU ZA WANAFUNZI:
Idadi ya wanafunzi waliojiunga na Chuo tangu mwaka 1415H / 995AD hadi mwaka 1425H / 2004AD imefikia wanafunzi 238 kutoka sehemu mbali mbali za Tanzania. Kati yao, wanafunzi 60 wamehitimu masomo ya sekondari, na 38 kati ya hawa wamepatiwa fursa ya kuendelea na masomo nchini Oman: 13 kati ya hawa 38 ni kutoka Tanzania Bara, 22 kutoka Pemba na 3 kutoka Unguja.
 

 

Maelezo zaidi kuhusu Chuo cha kiislamu na njia za kuweza kusaidia na kusponsa mwanafunzi tafadhali wasiliana na wanaokhusika na wasimamizi.

 

Copyright ©2005  Uislam.net