MTAZAMO WA KISHERIA

 KUHUSU  MASUALA TAFAUTI YA UKIMWI

(MISCELLANEOUS RELIGIOUS VIEWS ON AIDS)

ÈöÓúãö Çááåö ÇáÑøóÍúãäö ÇáÑøóÍöíúãö

ZANZIBAR CHILDREN’S FUND

ZCF

äóÏúæóÉ ÃóÆöãøóÉö ÇáãóÓóÇÌöÏö æóãõÏóÑøöÓöíú ÇáßóÊóÇÊöíúÈö ÇáÞõÑúÂäöíøóÉö ãöäú ßóÇÝøóÉö ãõÍóÇÝóÙóÇÊö ÇáÌóÒöíúÑóÉö ÇáÎóÖúÑóÇÁö Ýöíú ãõßóÇÝóÍóÉö æóÈóÇÁö ÇáÅöíúÏúÒ ÊóÍúÊó ÅöÔúÑóÇÝö ãõäóÙøóãóÉö ÑöÚóÇíóÉö ØõÝõæúáóÉö ÒöäúÌöÈóÜÜÇÑó

WARSHA YA MAIMAMU NA WALIMU WA MADRASA

KUTOKA WILAYA ZA PEMBA JUU YA

KUPAMBANA NA UKIMWI

MEI, 2005

ÇáãóäúÙõæúÑõ ÇáÔøóÑúÚöíøõ

Ýöíú ãõÎúÊóáóÝö ÇáãóÓóÇÆöáö ÇáãõÊóÚóáøöÞóÉö

 ÈöãóÑóÖö ÝõÞúÏóÇäö ÇáãóäóÇÚóÉö

((ÇáÅöíúÏúÒ))

MTAZAMO WA KISHERIA

 KUHUSU  MASUALA TAFAUTI YA UKIMWI

(MISCELLANEOUS RELIGIOUS VIEWS ON AIDS)

IMETAYARISHWA NA SHEIKH: KHALFAN SULEIMAN TIWANIY.

   KUTOKA TAWI LA ISTIQAMA,KUSINI-PEMBA.

UTANGULIZI:

Inaeleweka fika kuwa UKIMWI ni janga lililoikumba dunia yote;hasa ikizingatiwa kuwa maradhi haya hayana ubaguzi wala uchaguzi,humsibu yoyote yule pasi na kujali rangi yake,jinsia yake,dini yake,madhehebu yake,hali yake ya kiafya au ya kijamii,pia hayajali ucha-mungu wa mtu au uachaji-mungu wake,kwa kusema hivyo imekuwa ni kama jinamizi sugu linawarusha watu roho,kwa kutoa picha halisi si vibaya kama tukisema kuwa maradhi haya ni kama POPO-BAWA linapoingia mtaani hurufaisha nyoyo za watu wote,na labda ndio maana walimwengu wote waka”taharrak” katika ngazi za kimataifa na kitaifa na kukaa pamoja kujadili njia za kuutokomeza ugonjwa huu au kuupunguzia kasi yake ya uteketezaji na uangamizaji.

Kwa kuwa walimwengu wana imani kubwa na dini zao,na zaidi pale wanapofikwa na masaibu,kwa hivyo imeonekana kuwa dini ina nafasi kubwa katika kutekeleza jukumu hilo kupitia kwa viongozi wake katika mahafali zake tafauti,hususan kwa vile kujitokeza katika jamii zao masuala kadha yanayohitajiwa kupatiwa fatawa za kisheria.Hapa nimejaribu kukusanya baadhi ya masuala hayo  -angalia orodha mwisho -na kuyapatia ufumbuzi kwa mtazamo wa wataalamu wa sheria.

(1)-HUKUMU YA KUTUMIA MIPIRA (CONDOMS):

Mipira (Condoms)ni kitu kama soksi ya plastiki nyembamba ambayo huvaliwa katika uume wa mtu, ambayo huzuia kuanguka kwa maji ya uzazi katika ‘rahim’, condoms imekuwa ni kichochezi kizuri cha zina,Uislamu hauhamasishi kabisa utumiaji wa mipira hiyo ((ÇáÑøöÝóÜÜÇá)) hasa ukizingatia hadithi isemayo: ((ÇäúßöÍõæúÇ ÇáæóáõæúÏó æóÇáæóÏõæúÏó¡ÝóÅöäøöíú ãõßóÇËöÑñ Èößõãú ÇáÃõãóãó íóæúãó ÇáÞöíóÇãóÉö)) yaani: ((Oeni mwanamke mwenye kizazi,mwenye kupenda,kwani mimi nitajinata mbele ya uma nyengine (kwa wingi wa uma wangu) siku ya kiama)).

Hata hivyo itajuzu kutumia mipira hiyo katika hali za dharura zinazokubalika kisheria, kama vile mpango wa uzazi wa majira[1], au kwa kuhofia kuambukizana maradhi iwapo mmoja kati ya mume au mke kasibiwa na moja ya maradhi yanayoambukiza,na Allah ndie anayejua zaidi.

(2)-HUKUMU YA KUBEBA MIMBA KWA ALIYESIBIWA:

Dini ya Kiislamu inachunga kupatikana kizazi imara na inausia kufanya hivyo pindi ikiwezekana,amesema Mtume (s.a.w):

 ((ÇáãõÄúãöäõ ÇáÞóæöíøõ ÎóíúÑñ¡æóÃóÍóÈøõ Åöáóì Çááåö ãöäó ÇáãõÄúãöäö ÇáÖøóÚöíúÝö¡æóÝöíú ßõáøò ÎóíúÑñ)) yaani:((Muumini mwenye nguvu ni m-bora na anapendwa zaidi na Allah kuliko Muumini dhaifu,na wote wana kheri)).

Sasa ikithibiti kuwa kuna uwezakano mkubwa kwa Mama muathirika kuweza kubeba mimba salama basi itakua hakuna ubaya,kinyume cha hivyo itakatazwa kuchukua mimba,na Allah anajua zaidi.

(3)-HUKUMU YA KUHARIBU MIMBA KWA ALIYESIBIWA:

Kuharibu au kutoa mimba ((ÇáÅöÌúåóÜÇÖ)) kwa kuhofia kuwa mtoto alietumboni ataathirika kimaumbile kwa vile mama yake ni muhanga wa Aids ni kitu kisichokubalika, Allah S.W amepiga marufuku kuua,na mtoto akishapuliziwa roho,huwa ni nafsi iliyoharamika kuihiliki.Na kwa kuwa Allah ameshamleta basi hatuna njia ya kumuangamiza. Na mtu hana jukumu juu ya kile kilichoko tumboni na kinachotokea ndani yake kwani viumbe vyote vinasibiwa na mabalaa. Mtu huwajibika na hubeba jukumu pale anapokusudia uadui. Hivyo kuitoa mimba ni kufanya uadui,kwa hivyo atakayetoa mimba atawajibika kwa kitendo hicho mbele ya Allah.

(4)-HUKUMU YA MAINGILIANO YA KAWAIDA NA-ALIYESIBIWA:

Mtu aliesibiwa na maradhi ya Ukimwi ni kama mtu mwengine yoyote yule,ingawa Aids ni miongoni mwa maradhi yenye kuambukiza (Contagious deseases),lakini kwa vile njia za kuambukizana hazitokani na maingiliano ya kawaida (Casual contact) kwa hivyo itakuwa hakuna ubaya kushirikiana nae kimasomo, kibiashara na katika nyanja nyengine za kimaisha,na kama Mgonjwa kaathirika sana akawa anavuja kila pahala kiasi cha kutishia amani kwa wengine hapo atapaswa mgonjwa huyo kujitenga na watu ili asiwaambukize wengine,kasema Mtume (s.a.w): ((áÇó ÖóÑóÑó¡æóáÇó ÖöÑóÇÑó))

yaani:((Hakuna kujidhuru wala kudhuriana)),na Allah anajua zaidi.

(5)-HUKUMU YA MWENYE KUAMBUKIZA WENZAKE UGONJWA WA AIDS KWA MAKUSUDI:

Kitendo cha kumuambukiza kwa makusudi binaadamu mwenzako maradhi ya aina yoyote ni kitendo cha kinyama na cha kishenzi seuze uambukizaji wa Ukimwi, hili likitokea itaangaliwa,ikiwa kitendo  hicho kitapelekea kifo kwa upande wa pili basi hukumu ya kulipa kisasi itatumika na ikiwa si hivyo basi Hakimu ndio ataangalia adhabu gani inafaa kutiwa Mtendaji huyo, kwani hii itaingia katika hukmu ya  ((ÇáÊøóÜÚúÜÒöíÜúÑ)) na Allah ni mjuzi wa yote.

(6)-HUKUMU YA TOBA YA ALIEATHIRIKA:

Allah anapokea toba ya mja wake madhali haijafika wakati wa kutaka kukata roho na ndiyo akasema:

{Þõáú íóÇ ÚöÈóÇÏöíó ÇáøóÐöíäó ÃóÓúÑóÝõæÇ Úóáóì ÃóäÝõÓöåöãú áóÇ ÊóÞúäóØõæÇ ãöä ÑøóÍúãóÉö Çááøóåö Åöäøó Çááøóåó íóÛúÝöÑõ ÇáÐøõäõæÈó ÌóãöíÚÇð Åöäøóåõ åõæó ÇáúÛóÝõæÑõ ÇáÑøóÍöíãõ }ÇáÒãÑ53

yaani:((Waambie waja wangu waliofanya dhambi msikate tamaa na rehma ya Allah. Hakika Allah anasamehe dhambi zote kwani yeye ni mwingi wa kutoa misamaha na mwenye kurehemia)).

Pia imekuja katika hadithi kuwa:((Hakika Allah ananyoosha mkono[2] wake usiku ili kupokea toba kutoka kwa waliofanya madhambi wakati huo pia hunyoosha mchana kwa ajili ya watakaotenda dhambi kwa mchana huo)). na kunyoosha hapa imekusudiwa kukubali.. na Allah anajua zaidi.

(7)-HUKUMU YA KUMUUA ALIEATHIRIKA KWA HIARI YAKE KWA NIA YA KUMPUMZISHA!!:

Inaeleweka tosha kuwa Aids inatesa vibaya kiasi cha kuyatamani mauti,na katika miaka ya karibuni tu katika nchi za Ulaya ulitokezea mripuko wa baadhi ya madaktari kuwauwa magonjwa wanaosumbuliwa na maumivu makali kwa kuwatoga sindano za vifo kwa nia ya kuwapumzisha!

Maulamaa walilijadili suala hili kwa kina na wakaona kuwa ni haramu kuiua nafsi ya mtu pasi na haki, hata ikiwa ni kwa ridhaa yake,kasema Allah:

{..æóáÇó ÊóÞúÊõáõæÇú ÃóäÝõÓóßõãú Åöäøó Çááøåó ßóÇäó Èößõãú ÑóÍöíãÇð }ÇáäÓÇÁ29

yaani: ((Wala msiziuwe nafsi zenu hakika Allah kwenu ni mwenye rehema).

Na Mtume (s.a.w) amesema:

 {æóãóäú ÊóÍóÓøóì ÓõãøðÇ ÝóÞóÊóáó äóÝúÓóåõ¡ÝóÓõãøõåõ Ýöíú íóÏöåö  íóÊóÍóÓøóÇåõ  Ýöíú äóÇÑö Ìóåóäøóãó ÎóÇáöÏðÇ ãõÎóáøóÏðÇ ÝöíúåóÇ ÃóÈóÏðÇ}

yaani: ((..na atakaye kunywa sumu akajiua,sumu yake atakuwa nayo mkonono mwake anaichubua katika moto wa Jahannam milele na daima)).

Hivyo inapaswa mgonjwa wa Aids amche Allah na avumilie kwani kujiua kutampeleka katika adhabu kuu zaidi.

Pia waliosalimika wamvumilie mgonjwa aliyefikwa na mtihani huo, kwani Allah huwaonja kwa dhiki na shida na wengine kwa raha na neema.

N.B:Kwa maana hiyo Daktari akimtoga sindano ya kifo mgonjwa kwa makusudi itakuwa kauwa,na hivyo hivyo ikiwa atamtilia dawa ili ajiue..na Allah anajua zaidi.

(8)-HUKUMU YA KULEA MAYATIMA WA UKIMWI:

Uyatima ni kitu cha kisikitisha sana,hususan kwa jinsi jamii zinavyomtizama Yatima kama ni kiumbe kilichopungukiwa na mtunzaji,kwa hivyo mara nyingi Mtoto yatima huonewa na kudhulumiwa,Sheria ya Kiislaamu imelipa suala la mayatima kipa umbele sana,Mtume (s.a.w) amesema:

((ÃóäóÇ æóßóÇÝöáõ ÇáíóÊöíúãö Ýöíú ÇáÌóäøóÉ  ö ßóåóÇÊóíúäö)) æóÃóÔóÇÑó ÈöÃõÕúÈõÚóíúåö:ÇáÓøóÈóÇÈÉ óö æóÇáæõÓúØóì))

yaani:(Mimi na Mtunzaji wa Yatima  tutakuwa katika Pepo kama vidole hivi viwili, anasema hayo huku akiambatanisha kidole chake cha shahada na kile cha kati pamoja,pia Allah kawasimanga wale wanaowasuta mayatima kwa kusema:

{ÃóÑóÃóíúÊó  ÇáøóÐö í íõßóÐøöÈõ ÈöÇáÏøöíúäöó ÝóÐóáößó ÇáøóÐöí íóÏõÚøõ ÇáúíóÊöíãó }ÇáãÇÚæä2  

((Jee,umemuona yule anayekadhibisha dini,huyo ni yule anayemsuta Yatima..)).

Kwa ujumla suala la kuwatunza Mayatima katika dini lina umuhumi bayana,Yatima huyo awe wa karibu au wa mbali,huyo ni Yatima wa kawaida wachilia mbali Yatima wa Ukimwi ambaye anahitaji   matunzaji zaidi.. na Allah anajua zaidi.

(b):JEE INAFAA KULEA YATIMA WA UKIMWI WA ZINA?:

Kuna tetesi katika ndimi za watu kuwa mtoto wa zina ni muovu na hafai kuoa wala kuolewa na hatakasiki na uharamu wake mpaka kizazi chake cha saba (seventh generation),tetesi hizo zinaenezwa  kwa

kutegemea hadithi inayomsifu mtoto wa zina kuwa:

 ((åõæó ÔóÑøõ ÇáËøóáÇóËóÉö)).

yaani:(Yeye ni mbaya wa watatu)),ikimaanisha baina ya Mzinifu,Mama na Mtoto mwenyewe,na katika riwaya nyengine imekuja: ((æóáóÏõ ÇáÒøöäóÇ áÇó íóÏúÎõáõ ÇáÌóäøóÉó)) yaani: ((Mtoto wa zina haingii Peponi))...Lakini Watalamu wa Hadithi wamezidhoofisha hadithi hizi,kwani zinapingana na Aya za Qur-ani,kama ile aya isemayo:

{æóáÇó ÊóÒöÑõ æóÇÒöÑóÉñ æöÒúÑó ÃõÎúÑóì}

((Haitobeba nafsi madhambi ya nafsi nyengine)),na pia hadithi hizi zinapingana na akili,kwani kama ni makosa basi ni ya Wale wawili waliokubaliana kufanya ‘fahishatu-zinaa’ na sio ya Yule Mtoto aliyekuja bila ya khiari.

Kwa hivyo hakuna ubaya bali ni fadhila kubwa sana kumtunza mtoto wa aina hiyo,bali kuna malipo na Allah anajua zaidi.

(9)-HUKUMU YA NDOA YA WALIOSIBIWA:

Kisheria hakuna ubaya kwa waliosibiwa kuoana,hasa tukizingatia kuwa ndoa ina malengo mengi,kati ya hayo ni:

(a):Kujenga familia.

(b):Kukata shahwa.

(c):Kupata heshima katika jamii,n.k.

Na kwa vile ndoa ya wasibiwa itawakidhia haja zao,basi pia itachangia kwa kiasi kikubwa kutoenea kwa maradhi hayo mabaya kwa kupitia milango ya nyuma (unlawful sexual intercourse),kwa ajili hiyo hakuna kipingamizi cha sheria kuhusiana na ndoa hiyo.

(10)-HUKUMU YA KUDAI TALAKA KUTOKA KWA MUATHIRIKA:

Kama mwanamke atabaini kuwa mumewe kasibiwa na Aids mapema kabla ya yeye kuambukizwa,basi Wanavyuoni wameonelea kuwa ni haki ya mwanamke huyo kudai talaka yake,na kama mume atagoma kutoa talaka basi Mahkama itamuachisha kwa nguvu,kwani hii itaingia katika milango ya kifiqhi ya dosari zinazopelekea mke na mume kufarikiana[3]..Laa kama mwanamke ataridhia kuendelea na mumewe hivyo-hivyo ili kulea watoto wao pamoja basi pia inakubalika kisheria..na Allah anajua zaidi.

(11)-HUKUMU YA MAMA MUATHIRIKA KUMNYONYESHA MWANAWE:

Hapo nyuma ziliwahi kutoka fatwa kuwa hakuna ubaya kwa Mama muathirika kumnyonyesha mwanawe,kwa kutegemea Kanuni ya Kifiqhi isemayo: ((ÇÓúÊöÕúÍóÇÈ ÍóÇáóÉö ÇáÃóÕúáö)),yaani: ((Kwenda sambamba na hali ya asili)),lakini baada ya Sayansi ya Tiba kuthibitisha kuwa mama anamuambukiza mwanawe kwa njia ya kunyonyesha,kwa hiyo italazimika kutafuta njia nyengine kama vile kukodi Mnyonyeshaji au kutumia maziwa ya ng’ombe,mbuzi n.k. au maziwa ya makopo..na Allah ndie anaejua zaidi.

(12)-JEE UKIMWI UNA DAWA KWA MTAZAMO WA KISHERIA?:

Ukimwi ni maradhi, na kisheria inaaminika kikamilifu kuwa una dawa,imebakia kuwa haijajuilikana tu,hii ni kutokana na hadithi isemayo:

 ((ãóÇ ÃóäúÒóáó Çááåõ ÏóÇÁð ÅöáÇøó æóÃóäúÒóáó ãóÚóåõ ÏóæóÇÁð))

Yaani:((Allah hakuleta maradhi ispokuwa kaleta na dawa yake)),na katika baadhi ya riwaya imekuja:

 ((Úóáöãóåõ ãóäú Úóáöãóåõ¡æóÌóåöáóåõ ãóäú Ìóåöáóåõ))

((Ameijua alieijua,na hakuitambua aliekuwa-hakuitambua)),pia imekuja kwa lafdhi ya:

 ((áößõáøö ÏóÇÁò ÏóæóÇÁñ¡ÝóÅöÐóÇ ÃõÕöíúÈó ÏóæóÇÁõ ÇáÏøóÇÁö ÔõÝöíó ÈöÅöÐúäö Çááåö))

yaani: ((Kila maradhi yana dawa,na ikipatikana dawa ya maradhi,hupoa kwa idhini ya Allah)).

(13)- KUSHIRIKIANA NA WASIOKUWA WAISLAMU KATIKA KUPAMBANA NA JANGA HILI:

Ni jambo linaloeleweka tosha kuwa Uislamu ni dini iliyokamilika,na ina hukumu zake na hikma zake za kiiungu zisizoweza kubadilishwa,sasa vipi leo waislamu washirikiane na wasiokuwa waislamu katika kupambana na janga hili?

Hili ni suala nyeti ambalo hukanganya sana vichwa vya baadhi wa Waislamu..

Kwa ufupi suala hili itakuwa halina ubaya pindi ikiwa lengo ni kupambana na “adui fulani wa pamoja” ((ãõßóÇÝóÍóÉ ÇáÚóÏõæøö ÇáãõÔúÊóÑóßö)),vigezo vya jambo hili vinapatikana katika kitendo cha Mtume (s.a.w)alipoweka mkataba na Mayahudi kuilinda Madina kutokana na adui wa nje,pia pale alipomkodi Mushriki mmoja wa Makka kumpeleka Madina kupitia njia za kienyeji,na pia pale alipokuwa Madina mara nyengine alikuwa akiwaandikia barua baadhi wa Washrikina wa Makka wamzawadie Maji ya Zamzam,na Allah ndie ajuaye zaidi.

(14)-SUALA LA KUPIMA KABLA YA NDOA:

Hapana shaka njia moja itakayopelekea kupunguza uzagaaji wa maradhi ya Aids kwa wingi ni suala la kupima kabla ya kufunga ndoa,na kwa vile suala la afya lina nafasi kubwa katika dini,kwa nini isiwe kupima ni sheria ya lazima kabla ya ndoa? Wengine hudadisi.

Jawabu ni kuwa ndoa ina sharti zake maalumu za kusihi kwake,na suala la kupima halimo katika sharti hizo,lakini Kiongozi wa nchi akiona kuna maslaha ya kulipa suala hili uzito basi nafasi hiyo iko wazi katika dini hasa tukizingatia zile kawaida (laws)za kifikhi zisemazo: ((ãóÇ áÇó íóÊöãøõ ÇáæóÇÌöÈõ ÅöáÇøó Èöåö¡Ýóåõæó æóÇÌöÈñ ãöËúáõåõ)) yaani: ((Wajibu isioweza kutimia ispokuwa kwa kupatikana kitu Fulani,basi kitu hicho pia itakuwa kuna uwajibu kupatikana)),kwa maana ikiwa hatutowezo kuokoa maisha ya wanaotaka-kuoana ispokuwa kwa kuwapima basi itabidi kuwapima,na kaida nyengine ni ile isemayo: ((ÇáÖøóÑõæúÑóÇÊõ ÊõÞóÏøóÑõ ÈöÞóÏóÑöåóÇ)),yaani: ((Dharura zinaangaliwa vile zilivyo)),kwa maana ikiwa itakuwa ni mtindo wa watu kuambukizana maradhi wakati wa ndoa basi sheria inaweza kuchukua hatua zinazofaa kuhusiana na upimaji kabla ya ndoa.

(15)-MWENYE AIDS ATIZAMWE KWA JICHO GANI?:

Awali hatuna budi tufahamu kuwa Aids ni maradhi yanayoweza kumsibu mtu yoyote na kwa wakati wowote,huwapata wengine kama ni adhabu,amesema Allah: ((æóãóÇ ÃóÕóÇÈóßõãú ãöäú ãõÕöíúÈóÉò¡ÝóÈöãóÇ ßóÓóÈóÊú ÃóíúÏöíúßõãú)),yaani: ((Msiba wowote utakaokupateni ni kwa yale yaliyochumwa na mikono yenu)),na kwa ile hadithi isemayo:

 ((ãóÇ ÙóåóÑó Ýöíú Þóæúãò ÇáÒøöäóÇ Ãóæú ÇáÑøöÈóÇ ÅöáÇøó ÃóÍóáøõæúÇ ÈöÃóäúÝõÓöåöãú ÚóÐóÇÈó Çááåö)),yaani: ((Haitodhiri katika jamii zina au riba ela hujisababishia adhabu ya Allah)).

Na wengine hupatwa na maradhi haya kama ni mtihani ili Allah awalipe kheri pindi wakifanikiwa,kasema Bwana Mtume (s.a.w.):

 ((ãóäú ÃóÑóÇÏó Çááåõ Èöåö ÎóíúÑðÇ íõÕöÈú ãöäúåõ))

yaani: ((Anaemtakia Allah kheri basi humuonja kwa mitihani)).

Kwa hivyo si busara kumtazama aliesibiwa kama ni mzinifu,na hata kama itathibiti hivyo haina maana ya kuacha kumpa nasaha na kumuwaidhi na kumuombea hidaya,tukiangalia sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) utakuta alikuwa akiwafanyia ihsani wale waliokuwa wakimkera,na hata Qur-ani imewaekea wale watu waliokuwa na imani dhaifu fungu la zaka ili kuimarisha imani zao,wao walijuilikanwa kwa jina la ((ÇáãõÄóáøóÝóÉõ ÞõáõæúÈõåõã)) ,na imekuja katika athari kwamba Mtume (s.a.w.)alikua akiomba dua kwa kusema:

 ((Çááøóåõãøó ÃóÚöÒøó ÇáÅöÓúáÇóãó ÈöÃóÍóÏö ÚõãóÑóíúäö)),yaani: ((Yaa-Rabbi,Upe nguvu uislamu kwa mmoja kati ya Omar wawili[4])),akimaanisha Omar ibnul-Khatt’aab au Amruu ibnu Hishaam (Abu jahli),dua ikajibiwa akasilimu Omar bin Khatt’aab.

Siasa hii ndio iliyopelekea leo Uislamu kuwa na mamilioni ya wafuasi la si-hivyo dini hii ingalipotea..Tabaan,Mzinifu akidhihirisha inadi na uadui basi hadithi ziko nyingi zinazofahamisha namna ya kumtendea.Inatosha kutaja hadithi moja katika mnasaba huu,ni ile inayosema:

 ((ãóäú ÑóÃóì ãöäúßõãú ãõäúßóÑðÇ ÝóáúíõÛóíøöÑúåõ ÈöíóÏöåö¡ÝóÅöäú áóãú íóÓúÊóØöÚú ÝóÈöáöÓóÇäöåö¡ÝóÅöäú áóãú íóÓúÊóØöÚú ÝóÈöÞóáúÈöåö¡ æóÐóáößó ÃóÖúÚóÝõ ÇáÅöíúãóÇäö)) yaani: ((Yoyote atakayeona ubaya basi na auondoshe kwa mkono wake,ikiwa hakuweza augeuze kwa ulimi wake na kama hakuweza basi kwa moyo wake,na huo ni udhaifu wa Imani))..na kuna aya nyingi za Qur-ani zinazoweza kutumika katika mnasaba kama huu..Wallahu A’alam.

(16)- UMUHIMU WA HABARI KATIKA UISLAMU:

Yoyote anayefahamu yaliyomo katika Qur-ani japo kidogo atajua umuhimu wa habari katika Uislamu,inatosha kukumbuka kisa cha Nabii Suleiman na Ndege wake “Hud-hud”, pia Qur-ani yote ni visa vya Mitume waliotangulia ambavyo kutokana na umuhimu wake Allah alimsimulia Mtume wake,akamwambia:

 ((äóÍúäõ äóÞõÕøõ Úóáóíúßó ÃÍúÓóäó ÇáÞóÕóÕó ÈöãóÇ ÃóæúÍóíúäóÇ Åöáóíúßó åóÐóÇ ÇáÞõÑúÂäó¡æóÅöäú ßõäúÊó ãöäú ÞóÈúáöåö áöãöäó ÇáÛóÇÝöáöíúäó)).

Kwa hivyo hapana budi Waislamu hasa Mashekhe na Walimu wa vyuo watumie nafasi zao kuelimisha jamii madhara ya majanga tafauti yanayotokea Ulimwenguni likiwamo suala la UKIMWI.

Êóãøó ÈöÍóãúÏöÇááåö .....ÃóÚóÏøóåõ áóßõãú ÎóáúÝóÇä Èúä ÓõáóíúãóÇä ÇáØøöÜÜíúÜÜæóÇäöÜÜíú

18/ÑÈíÚ ÇáËÇäí/1426åÜ ÜÜÜÜ 27/ãÇíæ/2005ã
 
    MASUALA YA KUJIPIMA

(1)-Kwa nafasi yako kama Imamu au Mwalimu,Jee unahisi kuna haja ya kuweka sheria ya lazima ya kupima Aids kabla ya ndoa,kama jawabu ndio au siyo,orodheza sababu zako.

 

(2)- Taja njia ambazo Maimamu na Walimu hutumia katika kulielezea suala la Ukimwi,na kwa kiwango gani hufanikiwa na yepi matatizo yanayowakumba katika kufanikisha suala hilo?

 

(3)- Kwa mtazamo wako,kwa kiwango gani Uislamu umechangia kupunguza janga la Ukimwi? Eleza kwa kifupi kwa njia ya madondoo.

 

ü      YALIYOMO

(1)-HUKUMU YA KUTUMIA MIPIRA (CONDOMS).

(2):HUKUMU YA KUBEBA MIMBA KWA ALIYESIBIWA.

(3):HUKUMU YA KUHARIBU MIMBA KWA ALIYESIBIWA.

(4):HUKUMU YA MAINGILIANO YA KAWAIDA NA ALIYESIBIWA.

(5):HUKUMU YA MWENYE KUAMBUKIZA WENZAKE KWA MAKUSUDI.

(6):HUKUMU YA TOBA YA ALIEATHIRIKA.

(7):HUKUMU YA KUMUUA ALIEATHIRIKA KWA HIARI YAKE NIA YA KUMPUMZISHA!!

(8):HUKUMU YA KULEA MAYATIMA WA UKIMWI.

(9):HUKUMU YA NDOA YA WALIOSIBIWA.

(10):HUKUMU YA KUDAI TALAKA KUTOKA KWA MUATHIRIKA

(11):HUKUMU YA MAMA MUATHIRIKA KUMNYONYESHA MWANAWE.

(12):JEE UKIMWI UNA DAWA KWA MTAZAMO WA KISHERIA?

 (13)-KUSHIRIKIANA NA WASIOKUWA WAISLAMU KATIKA KUPAMBANA NA JANGA HILI

 (14)-SUALA LA KUPIMA KABLA YA NDOA

 (15)-MWENYE AIDS ATIZAMWE KWA JICHO GANI?

 

Sayansi ya tiba mpaka sasa inaona kuwa mama muathirika hawezi kumuambukiza mwanawe kwa njia ya kumnyonyesha,kwa mintarafu hii itakuwa hakuna haja kisheria kumzuia mama kumnyonyesha mwanawe, hii inaingia katika sheria ((ÇÓúÊöÕúÍóÇÈö ÍóÇáóÉö ÇáÃóÕúáö)) ispokuwa pale tu Daktari atakaposhauri kutofanya hivyo kwa kuchunga mambo fulani-fulani,au kwa kuja tafiti mpya.. na Allah anajua zaidi.

 

(16)-NJIA GANI AMBAZO UISlAMU UMEZITOA KAMA NI SULUHISHO KATIKA KUTOKOMEZA AU KUPUNGUZA JANGA LA AIDS?

Kujihadhari na UKIMWI

 Endapo atapata vurusi vya ukimwi mmoja kati ya mume au mke bila kumjulisha mwenzake kuhusu ugonjwa

 ni njia ipi ya kufanya ili kuunusuru upande mwingine uliosalimika au kwa maana nyingine je, inafaa kukutana kimwili baina yao?

Jawabu: Bismillah Rrahmani Rrahiim. Kwa kweli katika Uislamu kinga ni jambo litakikanalo na ndio maana ya kuwekwa sheria kuchukua hadhari na kujikinga na njia zote zinazosababisha magonjwa na maangamizi. Imekuja katika hadithi amri ya kumkimbia (kumuepuka) mwenye ukoma kama namna umkimbiavyo simba na ziko hadithi nyingi zinazoelezea kuchukua hadhari ya ugonjwa wa kuambukiza. Hivyo anapaswa watu wote kujikinga na maradhikama haya.

 

Amesema Jabir bin Abdi-llah:

((ßõäøóÇ äóÚúÒöáõ Úóáóì ÚóåúÏö ÑóÓõæúáö Çááåö Õóáøóì Çááåõ Úóáóíúåö æóÂáöåö æóÓóáøóãó æóÇáÞõÑúÂäõ íóäúÒöáõ¡æóáóæú ßóÇäó ÔóíúÆðÇ íõäúåóì Úóäúåõ áóäóåóì Úóäúåõ ÇáÞõÑúÂäõ)).

yaani: ((Tulikuwa tukimwaga nje wakati wa Mtume (s.a.w) na Qur-ani inateremka,na ingalikuwa ni jambo la kukatazwa ingalilikataza Qur-ani)),maneno haya yanatoa mwanga[5] kuhusiana na matumizi ya


[1] - Uzazi wa majira unaokusadiwa hapa ni ule wa kutenganisha baina ya mimba na mimba kwa lengo la kuhifadhi afya na mama na hata afya ya watoto,na sio ule wa kuweka idadi ya watoto kama wawili au watatu.

Vile-vile suala la kuruhusu kueneza Condom kiholela linabashiria shari kubwa katika jamii.

[2] - Kunyoosha mkono hapa ni kinaya ya kupokea toba,kwani Allah hana viungo wala hajafanana na kiumbe chochote,Yeye ndie aliyesema: ((áóíúÓó ßóãöËúáöåö  ÔóíúÁñ)).

[3] - N.B:Gazeti moja maarufu la Misri lilitawanya Fatwa ya Mufti Mkuu wa Nchi hiyo Sh.Nasr Farid Wassel inayosema kuwa Sigara ni katika madhambi makuu,na kutokana na madhara yake kuwa ni mabaya na yenye kudhuru wengine ameoneleo kuwa ni haki kwa mke kudai talaka kutoka kwa mumewe mvutaji,alikaririwa akisema: ((Madhara yatakayosababishwa na Talaka hayawezi kuzidi bali hata kufikia nusu ya madhara yanayosababishwa na Sigara)),Sh.Farid aliwahi kutunukiwa zawadi na WHO ((ãõäóÙøóãóÉõ ÇáÕøöÍóÉö ÇáÚóÇáóãöíøóÉö)) kwa jitihada zake za kupambana na Sigara.

Fatwa hiyo imezua kivumbi nchini Misri baina ya wanaoikubali na wanayoipinga,lakini ukweli utabaki ni ukweli kuwa sigara ina madhara makubwa.

Nchi nyingi za Kiarabu ni lazima katika kila pakti ya sigara kuwe na ibara ifuatayo:

 ((ÊóÍúÐöíúÑñ Íõßõæúãöíøñ:Åöäøó ÇáÏøõÎóÇäó ÓóÈóÈñ ÑóÆöíúÓöíøñ áöÃóãúÑóÇÖö ÇáÑøöÆóÉö æóÇáÓøóÑóØóÇäö æóÇáÔøóÑóÇíöíúäö æóÃóãúÑóÇÖö ÇáÞóáúÈö))

yaani: ((Tangazo la Serikali:Sigara ni sababu kuu ya maradhi ya mapafu,kensa, kuziba mishipa ya damu,na maradhi ya moyo)).

Matangazo yanayofanana na hayo yameanza kuonekana katika mabango ya njiani katika Jiji la Dares-Salaam.

[4] - Hapa wameitwa Omar wawili pamoja na kuwa ni Omar na mwengine ni Amruu,hili linakubalika katika Lugha ya kiarabu,hasa ikiwa vitu viwili hivyo vinafanana katika sifa Fulani,kwa mfana Jua (Shamsu) na Mwezi (Qamar) yanaitwa katika Kiarabu: ((Qamaraini)).

[5] - Nataka kusema kuwa Izali ilikuwa inawatimizia malengo yao ya kutochukua mimba,lakini wakati huo-huo ikiwakosesha raha nyengine za kimwili na ingalikuwa tayari “condom” zimeshavumbuliwa basi wengalizitumia kupata yote.

 

Copyright ©2005  Uislam.net