|

SALA YA TARAWEEH
1) HUKUMU YAKE:
Sala ya
Taraweeh ambayo pia huitwa sala ya kisimamo cha Ramadhan (Salat L’Qiyam) ni
katika Sunna amabazo inatakiwa Muislamu azitilie umuhimu na kutozipuuza.
Mtume wetu Muhammad (S.A.W)alisali sala hii ya Taraweeh na masahaba zake
sala ya jamaa baaadhi ya siku za Ramadhani, kasha hakuendelea baada ya hapo
kuisali jamaa alikhofia isije ikafaridhioshwa. Na sala hii ni Sunna sio kama
wanavyosema baadhi ya watu kuwa ni faridha ila anae acha kuisali anahesabiwa
yuko duni katika daraja.
2) WAKATI WAKE:
Husaliwa
baada ya sala ya Ishaa katika siku za mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Wakati wake huanzia baada ya sala ya Ishaa
mpaka kabla ya adhana ya Al-fajiri. Na utaratibu wa kusali sala hii ni
kwanza kusali sala ya Ishaa rakaa nne, kisha Sunna ya Isha rakaa mbili.
3) IDADI YA RAKAA KATIKA SALA YA TARAWEEH:
Mtume (S.A.W) alisali sala hii rakaa nane. Abubakar (Allah
awe radhi juu yake) wakati wa ukhalifa wake aliongeza rakaa nane nyingine
zakawa rakaa 16, na Omar bin Alkhattab (Allah awe radhi juu yake) wakati wa
ukhalifa wake pia aliongeza rakaa nane nyingine zikawa rakka 24. Na hizi
rakaa walizoengeza ni ziada kutoka kwa Makhalifa hawa wawili; Abubakar na
Omar (Allah awe radhi juu yao). Hii ni dalili ya kuwa sala ya Taraweeh upo
uwezekano wa kuongeza idadi ya rakaa isipokuwa ni bora zaidi kumfuata Mtume
Muhammad(S.A.W) amabe aliisali sala hii rakaa nane.
Kisimamo (Qiyam) kimoja katika sala ya Taraweeh ni rakaa nne.
Na unaweza ukasali sala hii kwa kisimamo (Qiyam) kimoja au viwili au vitatu
inategemea uwezo wako. Na baina ya visimamo (Qiyam) viwili (baada ya rakaa
nne), unamdhukuru Allah na kuomba Duaa.
Na ndio maana sala hii ikaitwa “QIYAM RAMADHAN”. Katika
wakati huo unaweza kumdhukuru Allah kama ifuatavyo:
SUBHAANA LLAH, WAL
HAMDU LILAH, WALA ILAHA ILLA LLAH, WALLAHU AKBAR, WALILAHI LHAMD. ADADA
KHALQIHI WAZINAT ARSHIHI WAMIDAADA KALIMATIH WARIDHAA NAFSIHI WAKAMA
YANBAGHI LAHU WAKAMA HUWA LAHU AHL LA YANQATIU WALA YANFADU MIN AZALI L’AZAL
ILA ABAD L’ABAD. WA SALA LLAGHU WASALAM ALAA SAYYIDNA MUHAMMAD WA ALAA ALIHI
WASAHBIHI AJMAIIN.
4) VIPI HUSALIWA:
I) RAKAA YA KWANZA
Fanya yafuatayo:
a) Soma
Tawjeeh
(SUBHAANAKA LLAHUMA,
WABIHAMDIKA, TABAARAKA S’MUKA, WATAALA JADUKA, WALA ILAHA GHAIRUKA. INNI
WAJJAHTU WAJHIYA LILLADHI FATTARA SAMAAWAATI WAL ARDHA HANIIFAN WAMAA ANAA
MINA L’MUSHRIKIIN).
b) Piga Takbiratul Ihraam (Allahu Akbar)
c) Soma Istiadha kutokana na shetani
(audhubillahi mina shaytani
rajeem)
d) Soma Suratil Faatiha na kisha soma sura yeyote katika
Quran, na inapendekezwa kusoma sura ndefu.
e) Rukuu kisha sujudi.
II) RAKAA YA PILI
Fanya yafuatayo:
a) Soma Al Fatiha na surah
b) Rukuu na sujudi
c) Kaa Tashahhud (kukaa tahiyyat), soma tahiyyat
(Attahiyyaatu lillahi wassalawaatu wattayyibaatu. As’salamu
alayka ayyuha nnabiyyu warahmatu llahi wabarakaatuh. As’salamu alayna wa
alaa ibadi llahi ssaalihin. Ash’hadu an’laa Ilaaha illa llah wa ash’hadu
anna Muhammadan abduhu warasuluh.
d) ToaTaslim (kutoa salaam)
III) RAKAA YA TATU
Inuka
rakaa ya tatu bila takbira, Katika hii rakaa fanya kama ulivyofanya katika
rakaa ya kwanza. Soma tawjeeh(SUBHAANAKA
LLAHUMA, WABIHAMDIKA, TABAARAKA S’MUKA, WATAALA JADUKA, WALA ILAHA GHAIRUKA,
takbiratul ihraam, istiadha, soma suratil Faatiha na sura nyingine.
IV) RAKAA YA NNE
Fanya kama ulivyofanya katika rakaa ya pili lakini atahiyyat
unaimaliza mpka mwisho
(Attahiyyaatu lillahi
wassalawaatu wattayyibaatu. As’salamu alayka ayyuha nnabiyyu warahmatu llahi
wabarakaatuh. As’salamu alayna wa alaa ibadi llahi ssaalihin. Ash’hadu
an’laa Ilaaha illa llah wa ash’hadu anna Muhammadan abduhu warasuluh.
Allahuma Sali alaa Muhammad wa alaa aali Muhammad kama sallayta alaa Ibrahim
wa alaa aali Ibrahim, wabaarik alaa Muhammad wa alaa aali Muhammad kama
baarakta alaa ibrahim wa alaa aali Ibrahim fil aalamina innaka hamiidun
majiid. Na baada ya
salaam unakaa kumdhukuru Allah na kuomba dua. Hapa inakuwa tayari umemaliza
kisimamo (Qiyam) cha kwanza.
Hukumu ya Duaa Baada Ya Kila Rakaa Nne (baada
ya kila Qiyam):-
Dua zinazoombwa baada ya taraweeh si lazima wala si moja
katika yanayotakikana kufanywa katika salaa. Lakini inapendekezwa kumuomba
Allaha baada kila salaa. Kama alivyosema allah Taala:
(ÝóÅöÐóÇ
ÝóÑóÛúÊó ÝóÇäÕóÈú æóÅöáóì ÑóÈøößó ÝóÇÑúÛóÈú)
BASI UKISHAMALIZA (KULINGANIA) SHUGHULIKA (KWA IBADA) NA JIPENDEKEZE KWA
MOLA WAKO (94: 7-8)
Watu husoma dua baada ya kila rakaa nne katika taraweeh kwa
kusoma albaqiyatul swalihat
SUBHAANA LLAH, WAL
HAMDU LILAH, WALA ILAHA ILLA LLAH, WALLAHU AKBAR, WALILAHI LHAMD. ADADA
KHALQIHI WAZINAT ARSHIHI WAMIDAADA KALIMATIH WARIDHAA NAFSIHI WAKAMA
YANBAGHI LAHU WAKAMA HUWA LAHU AHL LA YANQATIU WALA YANFADU MIN AZALI L’AZAL
ILA ABAD L’ABAD. WA SALA LLAGHU WASALAM ALAA SAYYIDNA MUHAMMAD WA ALAA ALIHI
WASAHBIHI AJMAIIN. Na
kufanya hivyo si lazima lakini inapendekezwa.
5) KUMBUSHO (Tanbih)
A) Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa
kubwa ya kuongeza kwa wingi thawabu zako kwani thawabu zake ni kubwa kuliko
miezi mingine. Tumia fursa hii wala usiiharibu au kuipoteza kwa mambo
yasiyokuwa na faida kwako.
B) Allah wa RamadhanI ndiye huyo wa
Shaaban na miezi mingine. Jitihada yako ya ibada isiwe katika Ramadhani tu
bali iwe ni jitihada ya kuendelea katika miezi yote ya mwaka.
C) Inajuzu mwanamke muislamu kusali
taraweeh jamaa nyuma ya imamu kwa sharti; asali mistari ya nyuma, avae
mavazi ya kusitiri mwili wake wote bila ya kuonyesha viungo na asipake
mafuta mazuri ya kunukia. Siku
hizi zipo sehemu misikitini za kusalia wanawake. Mwanamke akisali nyumbani
kwake ni bora lakini akitaka kusali Taraweeh jama na imam msikitini basi
hakatazwi.
D) Usitie mkazo na bidii kusali nawafil na
sunna kama vile Taraweeh halafu ukapuuza sala za faridha na pia kuchelewa
kwenda kusali sala ya alfajiri jamaa.
E) Baadhi ya watu hudhania kuwa rakaa za sala
ya Taraweeh zimeungana na zinaendelea. Wanaosali husimama baada ya rakaa ya
pili kuingia ya tatu kwa kutoa takbira na huiacha takbiratl ihraam katika
rakaa ya tatu pamoja na kuwa wametoa salaam baada ya rakaa ya pili na hili
ni kosa. Na iliyokuwa sawa ni baada ya kutoa salaam katika rakaa ya pili
unasimama kuingia rakaa ya tatu bila ya takbir. Halafu unasoma tawjeeh
kisha unatoa takbiratul ihraam.
F) Baadhi ya watu husali sala ya taraweeh
mbio mbio ili wakamilishe rakaa ishirini. Ni bora kusali rakaa nane kwa
utulivu kuliko kusali rakaa ishirini mbio mbio. Kwa sababu kusali kwa
utulivu inakutia utulivu (khushuu) katika sala yako. Na utulivu ndio roho
ya salaa.
G) Ikiwa muislamu atachanganya sala (ikiwa
amesafiri), ya maghrib na ishaa kwa kuzisali zote wakati wa magharibi (jamaa
taqdiim), inafaa kusali salatil taraweeh baada ya sala ya magharibi na
ishaa. Na pia ikiwa atachanganya sala ya magharibi na ishaa kwa kuzisali
zote wakati wa sala ya ishaa (jamaa taakhir), inafaa kusali sala ya taraweeh
baada ya kusali magharibi na ishaa.
H) Na mwisho, ndugu yangu muislamu, kumi la
mwisho katika mwezi mtukufu wa ramadhani uko usiku ambao ni bora kuliko
miezi elfu moja. Usiku huo ni Laylatul qadr. Kazania sana kufanya ibada na
kumdhukuru Allah katika siku hizo kumi. Kumi la mwisho si wakati
wakushughulika na kujitayarisha na siku kuu ya Eid. Utakuwa umeipoteza
fursa kubwa sana ikiwa kama hutoshughulika na ibada.
|