|
HUKUMU
ZA SIKU YA 11, 12, NA 13 DHUL-HIJA
-Kulala Mina siku za
tashriq ni sunna iliyowajibishwa; asiyelala huko itamlazimu kuchinja.
-Kulala kuliko lazima ni
usiku wa kuamkia tarehe 11 na 12 kwa wenye haraka. Ama wasio na haraka ni
usiku wa wa kuamkia tarehe 11, 12 na 13.
-Inasuniwa
kukithirisha takbir katika siku hizi katika kila hali.
-Mwenye kuhiji atazipiga
jamra tatu kila siku katika siku za tashriq kwa vijiwe ishirini na moja kila
jamra vijiwe saba.
-Ataanza
kulipiga jamra dogo, kisha la kati, kisha jamra kuu.
-Kupiga
jamra siku hizi huwa baada ya kupindukia jua (adhuhuri) mpaka kutua jua,
ikiwepo nafasi.
-Ataomba dua baada
ya kupiga jamra dogo na la kati, na haombi dua baada ya jamra kuu kutokana
na alivyofanya Mtume - rehema za Allah na amani zimshukie.
-Atazipiga
tena jamra tatu kwa mpanglio huu katika siku mbili zilizobaki kwa asiye na
haraka, na katika siku ya pili kwa mwenye haraka.
-
Mwenye kutaka kuharakiza kuondoka Mina
itamlazimu atoke kabla kuzama jua; akichelewa atabaki mpaka siku inayofuata.
TAWAFU
YA KUAGA:
_ Mwenye kuhiji akimaliza
kuzipiga jamra akataka kusafiri anapaswa aje kwenye Nyumba Takatifu atufu
tawafu ya kuaga mizunguko saba.
_ Tawafu ya kuaga ni
sunna iliyowajibishwa; mwenye kuiacha itamwajibikia kuchinja, isipokuwa
mwenye hedhi na mwenye nifasi inawajuzia kuiacha.
_ Hapana ubaya katika
kumbeba mgonjwa katika tawafu.
MAZINGATIO:
Atakayetufu tawafu ya kuaga na hakutimiza mizunguko saba inamlazimu kurudia
tena tawafu yake. Asipoirudia mpaka akatoka Maka itamwajibikia kuchinja.
Akitaka mwenye kuhiji kupumzika katika kutufu kutokana na msongamano mkubwa
au machofu hapana kitu juu yake, na itampasa aendelee alipofika katika
tawafu yake ikiwa hajatengua udhu wake; ukitenguka atatufu tena upya baada
ya kutawadha.
Hapana ubaya kwa aliyekwisha kutufu tawafu ya kuaga iwapo atakula au kunywa
bila kununua; analozuiliwa ni kuuza na kununua.
Inajuzu kwa aliyekwisha kuiaga Nyumba Takatifu kusali hapo hata nafla (sunna),
vilevile kuwasiliana kwa simu na kununua anachokihitaji katika safari ikiwa
ni petroli au kinginecho ikimbidi. Hivyo mwenye kununua viatu asivyo budi
navyo hapana kosa juu yake.
Inajuzu kuiaga Nyumba Takatifu kabla sala ya Ijumaa hata
kama ataondoka baada ya sala ya Ijumaa. |