|
Assalam Alaykum Warahmatullah Wabarakatuhu. Baada
ya kumshukuru Mwenyezi Mungu na kumtakia rehma Bwana Mtume Muhammad S.A.W. Ama
Baad: Hili ni jawabu la suala aliloulizwa Mheshimiwa Mufti Mkuu wa Oman. Sheikh
Ahmed bin Hamed Al-Khalili kuhusu toba ya mzinifu, Suala hili liliulizwa baada
ya kuzuka fatwa isiyokuwa ya kweli kwamba mzinifu hana toba, lazima
ajitambulishe na apigwe bakora, au atakuwa hana toba, ili watu wawe wazi
katika maarifa ya Dini yao, wanapaswa kuchukuwa Fatwa kwa Maulamaa waliosoma sio
kila apitae njia, na kujisemea bila ya elimu. Tafadhalini someni kwa makini na
isambazeni fatwa hii ili watu waijue.
  
|